Posts

Showing posts from December, 2019

Ajinyonga kwa msongo wa mawazo

Image
HAROUN Abdalla Faki (30) amekutwa amejinyonga huko Bububu Kijichi Mkoa wa Mjini Magharibi huku ikidaiwa chanzo chake kukabiliwa na msongo wa mawazo. Mmoja wa ndugu wa familia, aliyejitambulisha kwa jina mmoja, Juma alisema Faki alifika Bububu Kijichi kwa mjomba wake kwa ajili ya matembezi ya kawaida. Hata hivyo, kwa muda wa wiki moja alionekana akiwa na wasiwasi na mtu asiye na furaha muda mwingi, sawa na mtu aliyekumbwa na msongo wa mawazo. Akielezea tukio hilo, mtu huyo alikutwa akiwa tayari amejinyonga kwa kutumia shuka. “Haroub alifika Bububu Kijichi kwa mjomba wake kwa ajili ya matembezi ya kawaida ingawa kwa muda wote hakuwa na furaha akiwa sawa na mtu anayeonekana kuwa na msongo wa mawazo,” alisema. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Awadh Juma Haji alithibitisha tukio hilo na kuwataka vijana kuacha kutumia sheria mikononi mwao. Kwamba wanapokumbwa na misukosuko, wapate ushauri kwa watu husika. Alisema katika kipindi cha hivi karibuni, yamejitokeza matukio

Wabunge waliovuma mwaka 2019

Image
MWAKA 2019 umekwisha. Ulikuwa na mambo mengi katika medani za siasa kwa baadhi ya wabunge wa upinzani na chama tawala kujichanganya na ‘kuvuna walichopanda.’ Kwa upande wa chama tawala, wapo waliojichanganya kwa kushindwa kutumia vizuri ‘nyama ya ulimi,’ wakazungumza bila breki, lakini baadaye, wakatambua kosa lao; wakajitambua kuwa ni wana wapotevu; wakarudi nyumbani kwa baba na kuomba radhi. Uchungu wa mwana ajuaye mzazi; Rais John Magufuli akawasamehe. Hao, ni January Mamba, Nape Nnauye na William Ngeleja wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kwa upande wa upinzani, uwajibikaji ukapungua kwa baadhi ya wabunge; wakashindwa kufanya kazi kwa mfumo rasmi na badala yake, wakataka kufanya kwa mazoea, bila kujali kwamba zama za kutenda kwa mazoea zimekwisha. Hao wakajikuta wanajivua ubunge bila kujua. Hao ni Joshua Nassari wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). MAGUFULI ANAWASAMEHE WABUNGE WALIOMSEMA VIBAYA Mwaka ulioisha wa 2019 umekuwa na mambo mengi ambapo kati ya mambo hayo ni

Aiba Kichanga Anusurika kifo

Image
Mama mmoja, mkazi wa Kitongoji cha Mwanzugi wilayani Igunga Mkoa wa Tabora aliyejifanya mjamzito, Shija Mihambo (32) amenusa kifo baada ya kupigwa na wananchi kwa tuhuma za wizi wa kichanga. Mganga Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Dk Deus Rutha alisema, tukio hilo wiki iliyopita muda wa saa moja asubuhi kwenye wodi ya wajawazito. Dk Rutha alisema, akiwa nyumbani kwake, alipigiwa simu na Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Igunga, Dk Merchades Magongo akimjulisha kuna wizi wa kichanga. Alisema alikwenda hadi hospitalini hapo ambapo alikuta wananchi wengi, huku mtuhumiwa akiwa tayari amekamatwa na mganga mfawidhi kwa kushirikiana na wananchi. Alisema mama huyo, alikamatiwa maeneo ya stendi kuu ya mabasi saa 1:48 asubuhi akiwa na kichanga hicho chenye uzito wa kilo 3.3 cha jinsi ya kike akiwa kwenye pikipiki aliyokodi kwenda Kitongoji cha Mwanzugi. Dk Rutha alimtaja mama aliyeibiwa mtoto kuwa ni Hoka Maganga, mkazi wa Kijiji cha Bulenya Kata ya Nanga ambaye alifika hospitalini

Waandamanaji wa Iraq wavamia ubalozi wa Marekani

Image
Waombolezaji nchini Iraq wamekusanyika nje ya ubalozi wa Marekani mjini Baghdad kulaani mashambulio ya ndege za Marekani yaliyolenga vituo vya wanamgambo wa Kishia. Waombolezaji hao walizingira ubalozi huo uliopo kwenye eneo lenye ulinzi mkali wakiwa wamebeba bendera za kundi la wanamgambo lenye ushawishi mkubwa. Wakati huo huo, Saudi Arabia imewalaani wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran kwa kuyashambulia majeshi ya Marekani yaliyoko nchini Iraq ambapo mkandarasi mmoja wa Marekani aliuliwa. Wanamgambo hao walifanya mashambulio hayo wiki iliyopita. Marekani ilijibu kwa kuwashambulia kwa ndege wanamgambo hao wa Kataib Hezbollah Jumapili iliyopita. Wanamgambo hao wa Hezbollah walikishambulia kituo cha kijeshi cha Marekani nchini Irak Ijumaa iliyopita. Hata hivyo Waziri Mkuu wa Iraq, Adel Abdul Mahdi ameilaani pia Marekani kwa kufanya mashambilio ya ndege yaliyolenga vituo vya wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran. Amesema hatua ya Marekani inaweza kuitumbukiza zaidi Iraq katik

Kigwangalla afunguka Baada ya Magufuli Kumpa Siku 5

Image
Baada ya Rais John Magufuli kuagiza Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Adolf Mkenda kumaliza tofauti zao vinginevyo atawaondoa, Kigwangalla ameibuka na kudai kuwa tayari walishamaliza tofauti zao na sasa hali ni shwari. Kupitia akaunti yake ya Twitter na Instagram  amesema walishafanya kikao na Katibu Mkuu, Prof. Adolf Mkenda cha kumaliza tofauti zao. “Kazi ya Urais ni ngumu sana, tulioteuliwa na Rais kumsaidia utendaji/usimamizi wa maeneo mbalimbali hatupaswi kumuongezea frustrations nyingine zaidi, sisi kwenye Wizara yetu, baada ya kikao na Chief Secretary tulimaliza tofauti zilizokuwepo na sasa hali ni shwari,” amesema Kigwangalla. Ni imani na heshima kubwa sana kwako kuteuliwa kuwa Waziri kwenye nchi yako. Kwenye nchi ya watu milioni 60, kwa nini Hamisi KIGWANGALLA? Sijui. Ni neema na baraka za Mungu tu. Maana siyo kila mtu kwenye maisha yake atapata fursa ya kuhudumu kwenye serikali kama Waziri ama kama Katibu

MAGAZETI YA LEO 1/1/2020

Image

Deni la Serikali laongezeka kwa asilimia 11

Image
Serikali imesema Deni la Serikali limeongezeka kwa asilimia 11 kutoka kiasi cha shilingi Trillion 49.84 katika miezi 6 ya mwazo ya utekelezaji wa bajeti ya serikali ya mwaka 2018/19 hadi kufika trillion 54.84 kwa kipindi cha miezi sita ya utekelezaji wa bajeti ya serikali kwa mwaka 2019/20. Akitoa tathimini ya utekelezaji wa bajeti ya serikali ya mwaka 2019/20 kwa kipindi cha miezi sita ya mwazo jijini Dodoma Waziri wa Fedha na Mipago, Dkt. Philip Mpango amesema deni hilo bado ni himilivu kulingana na viwango vya kimataifa ikiwamo kulingana na pato la Taifa. Amesema ukuaji wa Deni hilo ni kutokana na mikataba ya mikopo iliyoingiwa kipindi cha nyuma pamoja na mikopo ya riba nafuu kwa ajili ya ujenzi wa miradi mikubwa inayojengwa nchini. Katika ukuaji wa pato la Taifa Waziri Mpango amesema pato la taifa limekuwa kwa asilimia 6.9 ikilinganishwa na kipindi kama hicho kwa mwaka uliopita ukuaji huo ukichangiwa na ongezeko la michango ya ukuaji shughuli za kiuchumi na kuwanufaisha wal

TANROADS waombwa kuboresha barabara Simiyu

Image
Na James Timber-Simiyu Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amezipongeza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Simiyu kwa kazi nzuri zinazofanya na kuzisisitiza kutenga bajeti ya kuboresha ujenzi wa Barabara zote zinazounganisha Mkoa wa Simiyu na mikoa mingine ili zipitike wakati wote. Kiswaga ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Simiyu, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Desemba 30, 2019 mjini Bariadi ambapo amebainisha kuwa barabara zikiboreshwa zitarahisisha usafiri kwa wananchi na usafirishaji wa malighafi mbalimbali za viwanda na bidhaa zitakazozalishwa na viwanda, vinavyotarajiwa kujengwa Mwaka 2020. “Kazi inayofanywa na TANROADS na TARURA ni kazi ambayo inatia moyo  na itakuwa na mchango mkubwa kwa viwanda vya nguo, glasi na vifaa tiba vitakavyoanzishwa mwakani; kwa maana ya material(malighafi) itakayoingia na bidhaa zitakazotengenezwa zitasafirishw

Manchester United yaanza kubisha hodi nafasi za nne juu EPL

Image
Manchester United imeanza kubishia hodi nafasi ya nne kwenye Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kukamilisha mwaka 2019 kwa kishindo Jumamosi. Ilizamisha wenyeji Burnley 2-0 kupitia mabao ya Anthony Martial na Marcus Rashford uwanjani Turf Moor. Vijana wa kocha Ole Gunnar Solskjaer walijinyanyua kwa haraka baada ya kuchapwa 2-0 na Watford katika mechi iliopita na sasa wataingia mwaka 2020 na matumaini mapya wanaweza kufuzu kushiriki Klabu Bingwa Ulaya msimu ujao. Ili kutimiza ndoto ya kumaliza ndani ya mduara wa nne-bora, Martial na Rashford wataendelea kutegemewa na walidhihirisha umuhimu huo wao walipofungia United mabao katika mechi iliokuwa na nafasi chache sana nzuri za kufunga. Moja wapo ya vitu vizuri Solskjaer alishuhudia katika mechi hiyo ni kuwa kwa mara ya kwanza United haikufungwa bao baada ya kushindwa kufanya hivyo katika mechi 14 zilizopita.

Daraja kubwa zaidi laanza kutumia China

Image
Daraja la Pingtang Kusini mwa Jimbo la Guizhou nchini China lenye mnara mkubwa wa semiti duniani ilianza kutumika hapo jana. Daraja hilo liko katika eneo la Bouyei-Miao Jimbo la Qiannan, limeunganishwa na waya yenye urefu wa mita 2,135 kwenye korongo na itatumika kuunganisha barabara kuu ya Pingtang-Luodian . Jumla ya Yuan bilioni 1.5 (karibu dola milioni 215 za Kimarekani) ziliwekezwa katika ujenzi wa daraja hilo. Kufunguliwa kwa daraja hilo kutapunguza wakati wa kusafiri kati ya Pingtang na Luodian kutoka kwa zaidi ya saa mawili na nusu hadi karibu saa moja, na kuwezesha kuondoa umasikini katika maeneo yenye mwamba wa Gu.

Hakuna kuidhinisha matumizi kabla ya kutenga mikopo ya vijana, wanawake na walemavu - Dkt. Mabula

Image
Na James Timber-Mwanza Baraza la Madiwani la halmashauri ya manispaa  ya Ilemela limekubaliana kwa pamoja kutopitisha matumizi yeyote ya fedha za mapato ya ndani kabla ya kutenga asilimia kumi ya fedha hizo kwaajili ya mikopo ya wanawake 4%,  vijana 4% na watu wenye ulemavu 2%. Kauli hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula wakati akizungumza na wananchi wa kata za Ilemela, Kawekamo na Pasiansi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kuvitembelea vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu vinavyopatikana katika jimbo lake kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili katika sekta ya mikopo na kuzipatia ufumbuzi ambapo amesema kuwa Serikali imezielekeza halmashauri zote nchini kufungua akaunti maalumu kwaajili ya kuhifadhi fedha zitakazotumika kukopesha makundi hayo "Tumekubaliana katika baraza la madiwani hakuna kuidhinisha matumizi ya fedha zinazotokana na mapato ya ndani kabla ya kutenga fedha za mikopo  katika akaunti yake maalumu,"

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara yashika namba moja Kwa usafi

Image
Na John Walter-Manyara Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Manyara yanyakua Kikombe na Kitita cha shilingi Milioni Tatu baada kung’ara katika mashindano ya jumla ya Usafi na Mazingira na kuipiga chini Mikoa Mingine. Akikabidhi zawadi hizo kutoka ofisi ya wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto, Katibu Tawala wa mkoa wa Manyara Missaile Mussa amesema mashindano hayo yalihusisha Mikoa Mitatu Ya Manyara, Arusha na Katavi. Mkuu wa mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti amesema mkoa huo hausifiki kwa usafi tu bali katika Usalama na kila idara wapo vizuri. "Sisi sio watu wa maneno tunapiga kazi, ingekuwa ni mikoa mingine angezungumzia ushindi huu mwaka mzima' alisema Mnyeti. Naye  Katibu wa Afya mkoa wa Manyara Thomas Malle  anasema mafanikio hayo wameyapata kwa sababu wanazingatia kanuni zote za Usafi ambazo zinafanywa na kampuni walizozipa kazi.

VIDEO: Serikali yaweka kipao mbele sekta ya utalii, miundo mbinu kuboreshwa

Image
Katika kuimarisha sekta ya utalii Nchini serikali inaendeleza mpango wake wa kuboresha Miundombinu katika sekta hiyo ambapo ili kufanikisha suala hilo watanzania wametakiwa kutambua kuwa mchango wao ndiyo nguzo pekee katika kuchochea ukuaji wa utalii pamoja na  kujijengea utamaduni wa kutembelea maeneo hayo kwakua ndio tegemeo katika kutangaza vivutio vilivyopo katika maeneo yao. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USISAHAU KU SUBSCRIBE

VIDEO: RC MNYETI - ''sisi Mkoa wetu sio wa makelele kama mengine, tunafanya kazi

Image
Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Manyara yanyakua Kikombe na Kitita cha shilingi Milioni Tatu baada kung’ara katika mashindano ya jumla ya Usafi na Mazingira na kuipiga chini Mikoa Mingine. Akikabidhi zawadi hizo kutoka ofisi ya wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Katibu Tawala wa mkoa wa Manyara Missaile Mussa amesema mashindano hayo yalihusisha Mikoa Mitatu Ya Manyara,Arusha na Katavi. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USISAHAU KU SUBSCRIBE

VIDEO: Tetesi za soka leo Disemba 31

Image
Uongozi wa Yanga kwa kushirikiana na mabosi wa GSM, umekamilisha dili la mshambuliaji Ykipe Gnamien kwa kumpa dili la miaka miwili. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USISAHAU KU SUBSCRIBE

Kesi ya anayetuhumiwa kumuua na kumchoma moto mkewe upelelezi wakamilika

Image
Upelelezi wa kesi ya mfanyabishara Khamis Saidy, anayekabiliwa na mashtaka ya mauaji baada ya kumuua na kisha kumchoma moto mke wake Naomi Marijani, tayari umekwishakamilika. Hayo yameelezwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon ambapo ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo. Wakili Wankyo ameyasema hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Salum Ally, wakati kesi hiyo ilipofikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa, ambapo imepigwa kalenda hadi siku ya Januari 7, 2020, itakapotajwa tena. Ikumbukwe Mfanyabishara Khamis Saidy, anadaiwa kutenda kosa hilo Mei 15, 2019, nyumbani kwake maeneo ya Gezaulole Kigamboni, baada ya kumuua na kisha kumchoma moto wa magunia mawili ya mkaa mke wake na kisha kuyabeba mabaki ya mwili huo na kwenda kuyafukia shambani kwake Mkuranga.

Bashe asema Serikali haina mpango wa kufuta kilimo cha tumbaku

Image
Serikali haina mpango wa kufuta kilimo cha tumbaku nchini wala kuwapangia wakulima viwango vya uzalishaji kwa kuwa zao hilo ni miongoni mwa mazao yanayoliingizia taifa mapato makubwa. Naibu waziri wa Kilimo Hussein Bashe ameyasema hayo wakati akizungumza na wakulima wa tumbaku  wilayani Kahama na kudai kuwa changamoto ya wakulima kubaki na tumbaku imemalizika  baada ya serikali kutafuta wanunuzi kutoka katika maeneo mbalimbali duniani. Naye Mwenyekiti wa chama kikuu cha ushirika cha Kahama Bw. Emmanuel Charahani amesema ujio wa wadau na wanunuzi wapya umesaidia kuondosha hasara ya tumbaku iliyokuwa imekwama katika maghala na majumbani mwa wakulima.

Watu 12 wakamatwa na Polisi Mbeya wakiwa na Bangi

Image
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa 12 kutokana na tuhuma za kupatikana na dawa za kulevya (bhangi), pombe haramu ya moshi (gongo), mali za wizi na pombe kali zilizopigwa marufuku nchini. Watuhumiwa wamekamatwa katika misako na doria zinazoendelea Mkoani Mbeya katika kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka.  Watu hao walikamatwa mnamo Decemba 27, 2019 majira ya saa 15:00 Alasiri huko Kijiji cha Shigamba, Kata ya Utengule – Usongwe, Tarafa ya Usongwe, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya. Mtuhumiwa GADI CHARLES akiwa na miche ya bhan

Kiongozi Mstaafu wa Nissan akimbilia Lebanon

Image
Kiongozi Mstaafu wa Kampuni ya Nissan, Carlos Ghosn amekimbilia nchini Lebanon kutoka Japan alimokuwa akikabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya fedha. Hata hivyo amesema hajakimbia ili kuzuia haki isitendeke, bali ameyakimbia mashtaka ya kisiasa ambayo yanamkabili kwa sasa. Haijajulikana Carlos amewezaje kutoka ndani ya Japan kwa kuwa alikuwa amezuiwa kusafiri kutokana na masharti makali kwenye dhamana yake.

Antonio Nugaz awatuliza mashabiki Yanga kuhusu Niyonzima

Image
Baada ya ushindi wa bao 1-0 wa Yanga dhidi ya Biashara United, afisa muhamasishaji mkuu wa Yanga Antonio Nugaz ameweka wazi kuwa Yanga bado inafanya usajili mkubwa mmoja kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Pia ametangaza kuwa Niyonzima ataingia jijini Dar es Salaam Jumatano hii akitokea kwao Rwanda. “Mungua akijalia Jumatano chuma kinatua (Niyonzima) akishatua tutaambiana namna gani ya kumpokea, halafu kwamba kwa uzuri tumebakiwa na usajili mmoja mkubwa imebakia moja lazima aje mtu wa kuwalaza saa 12 na robo” amesema. Niyonzima anarejea Tanzania tena baada ya kuondoka mwanzo wa msimu 2019/20 kutokana na kuachwa na Simba SC aliyoitumikia kwa misimu miwili akitokea Yanga SC alikodumu kwa miaka sita mfululizo.

Picha: Wauaga mwaka kwa tukio la kuteleza juu ya barafu

Image
Mchanganyiko huu wa picha unaonyesha mashabiki wakishiriki katika kuteleza juu ya barafu katika hafla ya Toronto ya 2019 katika uwanja wa Bentway Skate huko Toronto, Canada. Mamia ya washiriki, walishiriki katika hafla hii ya kila mwaka inafanyika kuaga mwaka kwaheri kwa kuteleza juu ya barafu wakiwa wamejivalia mavasi yao ya kuoga Jumapili.