Posts

Showing posts from June, 2020

Prof. Ndalichako akagua miradi ya Elimu Kasulu, Kigoma

Image
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amekagua miradi ya elimu inayotekelezwa katika Halmashauri ya Kasulu mkoani Kigoma yenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 13. Miradi hiyo ni pamoja na  ujenzi wa Chuo cha Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi Kasulu, Chuo cha Ualimu Kabanga na jengo la Utawala la shule ya Sekondari Grand. Akizungumzia maendeleo​ ya ujenzi wa Chuo cha Ualimu Kabanga mara baada ya kukagua, Waziri Ndalichako amesema chuo hicho kinajengewa upya miundombinu yote​ baada ya ile ya awali kuchakaa sana na kushindwa kukarabatiwa. ​ Ameongeza kuwa ujenzi wa miundombinu ya​ chuo  hicho unagharimu zaidi ya bilioni 10, na kuwa utakapokamilika utabadili taswira ya mji huo kwa kuwa majengo yanayojengwa ni ya kisasa na imara ambayo yatadumu kwa muda mrefu. ​ Akizungumzia mradi wa ujenzi wa jengo jipya la utawala na utengenezaji wa mfumo wa maji katika shule ya sekondari ya Grand, Profesa Ndalichako amesema umegharimu zaidi ya Shilingi milioni 534 na kwa

Viongozi wawili CHADEMA wahamia TLP

Image
Wanachama wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wamekihama chama hicho na kujiunga na Chama cha Tanzania Labour (TLP), huku wakitoa sababu mbalimbali zilizowafanya wafikie uamuzi huo. Wanachama hao wamepokewa na kukabidhiwa kadi za TLP na Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Agustine Lyatonga Mrema, katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya chama hicho Magomeni Usalama jijini Dar es Salaam. Miongoni mwa wanachama hao ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA), Bibiana Benedict Dule Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, ambaye amesema amejiunga na chama hicho kutokana na msimamo wake wa kumuunga mkono wazi wazi Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli. Mwingine ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Ulinzi wa Chadema Kanda ya Serengeti Oscar Kaijage kutoka mkoani Shinyanga, ambaye pamoja na mambo mengine amesema amejiunga na chama hicho kutokana na kuvutiwa na utendaji kazi wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kueleza kuwa kwa hali y

Awesu ashangazwa na kadi nyekundu aliyopewa na mwamuzi

Image
KIUNGO wa Klabu ya Kagera Sugar, Awesu Awesu amesema kuwa hajui sababu ya kupewa kadi ya pili ya njano iliyomfanya atolewe nje jumla kwenye mchezo huo kwa kadi nyekundu. Yanga jana iliikaribiisha Kagera Sugar kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya robo fainali ambapo Kagera Sugar ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1. Bao pekee la Kagera Sugar lilifungwa na Awesu Awesu dakika ya 19 huku yale ya yanga yakijazwa kimiani na David Molinga dakika ya 52 na lille la ushindi likipachikwa kimiani na Deus Kaseke kwa mkwaju wa penalti. Awesu alionyeshwa kadi mbili za njano jambo lililofanya aonyeshhwe kadi nyekundu na mwamuzi wa kati jambo ambalo amesema kuwa hatambui sababu ya yeye kuonyeshwa kadi hizo. Awesu amesema:"Sikuongea jambo lolote kadi ya kwanza nikishangaa namna nilivyopewa nikasema sawa, kadi ya pili nilikuwa nimechezewa faulo nikawa namtoa mchezaji mwenzangu maana nilishajua amepanic nashangaa nakutana na kadi nyingine sijui ilikuaje, sijaongea jambo lolote na wala s

Macron: Ulaya itaendeleza mapambano ya ugaidi eneo la Sahel

Image
Viongozi wa kundi la nchi za Sahel na mshirika wao Ufaransa wameapa kusonga mbele na mkakati wa kupambana na uasi wa miaka nane wa makundi ya wanajihadi katika mkutano uliofanyika nchini Mauritania.   Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alikutana Jumanne na viongozi wa kundi la nchi za Sahel ambazo ni Mauritania, Burkina Faso, Chad, Mali na Niger. Mara baada ya mkutano huo uliolenga kutathmini mkakati mpya katika mapambano na makundi ya kigaidi, Rais Macron alisema kumekuwa na matokeo ya kushangaza kama vile kuyachukua maeneo kutoka mikononi mwa makundi ya kigaidi. "Muungano tulioutangaza huko Pau miezi sita iliyopita, uko tayari. Ulaya, taasisi zake na nchi wanachama, nchi jirani zote ziko tayari. Na ziko upande wenu kwasababu tunaamini ushindi unawezekana Sahel na hiyo ni sababu inayoamua utulivu wa Afrika na Ulaya," alisema rais Macron. Mkutano huo uliitishwa ili kuimarisha mbinu za kimkakati, zilizochochewa na mfululizo wa mashambulizi ya mwaka jana yaliyosababisha

Kocha wa Yanga amtimua Bernard Morrison kambini

Image
Kocha Mkuu wa Yanga SC Luc Eymael ameeleza masikitiko yake na kuamua kumuondoa kambini mchezaji Bernard Morrison aliyemleta Yanga January 2020 wakati anajiunga nao, Morrison kaondolewa kwa vitendo vya utovu wa nidhamu. “Nidhamu aliyoionesha kambini asubuhi hii (jana) nimeamua kumuondoa kambini sababu ya tabia yake sitaki kuzungumzia sana bahati mbaya sijui kapatwa na nini, toka nimerudi (likizo ya Corona) sijui kijana wangu (Morrison) niliyemleta hapa kapatwa na nini” “Nimeongea nae sana muda wote sijui hata kimemtokea nini hapa kama nilivyosema niliamua asubuhi hii (jana) kumuondoa kambini na club itatoa taarifa rasmi kuhusiana na hili”

Milioni 150 zajenga bwalo Nyasa

Image
SERIKALI ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli, imetoa Sh milioni 150 kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa bwalo na jiko, katika shule ya Sekondari ya Kilumba, Kata ya Lumeme Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma. Akitoa taarifa ya mradi huo kwa Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma, Kaimu Afisa Elimu Sekondari Halmashari ya Nyasa Oscar Elias amesema,  ujenzi wa Mradi huo umetekelezwa kwa kutumia Force account, ambao ulianza Septemba 20, 2019 na kukamilika Desemba 20 ,2019. “Mradi umetoa ajira za muda kwa watu 60, ikiwa ni wanawake 16 na wanaume 44. Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa na wananchi wa Kata ya Lumeme, tunaishukuru Serikali ya CCM kwa kutekeleza kwa vitendo Ilani ya Chama cha Mapinduzi’’,alisema. Akizungumza baada ya kukagua Mradi huo, Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Ruvuma Nuru Ngeleja, amesema Kamati ya Siasa ya CCM mkoa, imeridhishwa na utekelezaji wa mradi huo.  Ngeleja amewaomba wananchi siku ya uchaguzi Mkuu  kujitokeza kwa wi

Kamati ya CCM mkoa wa Ruvuma imekagua miradi mbali mbali ukiwemo wa chuo cha veta nyasa

Image
KAMATI ya Siasa ya CCM Mkoa wa Ruvuma imekagua mradi wa ujenzi wa  chuo cha ufundi stadi VETA Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma ambao unagharimu zaidi ya shilingi bilioni mbili. Akisoma taarifa ya mradi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nyasa,Jimson Mhagama  amesema mradi unahusisha majengo 16 na kwamba fedha za mradi zimepokelewa kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza zimepokelewa zaidi ya bilioni moja. Amesema mradi huo unatekelezwa  na mafundi mawili wakiwemo SUMA JKT ambaye anajenga majengo 14 na Simon Chiwanga ambaye anajenga vyumba viwili vya madarasa na kwamba mradi umetoa jumla ya ajira 123. Mhagama amesema mradi huo unatekelezwa kwa kutumia mtindo wa force account ambapo wananchi kutoka Kata ya Kilosa ambako mradi unatekelezwa wanashiriki  na kwamba mradi ulianza Februari 21,2020 na unaarajiwa kukamilika Julai 31 mwaka huu. Hata hivyo amesema mradi umefikia katika hatua tofauti za utekelezaji ambapo majengo saba yamefikia zaidi ya asilimia 80 ambayo ni nyumba ya Mkuu

Zaka zakazi ataja sababu ya Azam kukosa ubingwa

Image
Mkuu wa Idara ya Habari wa Azam FC, Thabit Zakaria 'Zakazakazi' amesema malengo ya klabu hiyo ni kushika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi licha ya kupitwa na wapinzani wao Yanga SC ambao anaamini wamekaa katika nafasi yake. Akifanya mahojiano maalumu  Zakazakazi amesema mipango yao ya msimu huu ni kumaliza nafasi ya pili kwakuwa Simba SC tayari imeshabeba ubingwa huku akiweka wazi sababu iliyopelekea wao kukosa ubingwa kuwa ni kutokana na kubadilishwa kwa makocha. Azam FC itajitupa dimbani kesho majira ya Saa 1:00 Usiku katika mtanange wa Robo Fainali ya Kombe la shirikisho dhidi ya Simba SC.

Zitto Kabwe amkaribisha Membe

Image
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe, amemkaribisha aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Mwanachama wa CCM Bernard Membe, kuunganisha nguvu kupitia vyama mbadala hii ni mara baada ya yeye kufukuzwa uanachama ndani ya CCM. Taarifa hiyo imetolewa kupitia ukurasa wa mtandao wa Twitter wa chama hicho hii leo Juni 30, 2020, ambapo imeandikwa hivi, "Ndugu yangu Bernard Membe kafukuzwa uanachama wa CCM, ninajua bado anatetea haki yake ya uanachama huko ni hatua sahihi, hata hivyo muda wa kuleta mabadiliko katika nchi umewadia, ninamsihi afanye maamuzi ya kuunganisha nguvu kupitia vyama mbadala" umeeleza ujumbe huo ambao umetolewa na Zitto Kabwe.

RC Shigela aipongeza TRA kuendesha kampeni ya elimu kwa Mlipakodi

Image
MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigela amesema kampeni ya elimu kwa mlipakodi inayoendeshwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) itawasaidia wafanyabiashara wanaokwepa kodi kuacha vitendo hivyo vya kuikosesha Serikali mapato. Shigela ameyasema hayo ofisini kwake alipotembelewa na maafisa wa TRA wanaofanya kampeni hiyo mkoani humo ambayo imelenga kuwaelimisha wafanyabiashara kuhusu masuala ya kodi ikiwa ni pamoja na kuwakumbusha kulipa kodi kwa wakati. Amesema kuwa, kuna baadhi ya wafanyabiashara wamekuwa wakikwepa kulipa kodi pengine kwa kujua au kutokua, jambo ambalo linahitaji elimu ya uelewa ili kila mwananchi afahamu wajibu wake kwenye ulipaji wa kodi kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Akiizungumzia kampeni hiyo, Shigela ameipongeza TRA kwa kuendesha zoezi hilo katika mikoa mbalimbali na kusema litaongeza ukusanyaji wa mapato baada ya wafanyabiashara kuelimishwa na kufahamu kuwa maendeleo ya nchi yanasababishwa na ulipaji wa kodi kwa ajili ya kubores

MAGAZETI YA LEO 1/7/2020

Image

Dkt Avemaria awashangaa wale wanaotembea na vyeti

Image
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Dkt Avemaria Semakafu, amewashangaa wale walimu walioweka vyeti vyao ndani kwa miaka minne bila kutafuta nafasi ya kujitolea kwenye shule zenye uhitaji na badala yake wamekaa kusubiri ajira kutoka Serikalini. Dkt Semakafu ametoa kauli hiyo leo Juni 30, 2020, kuwa walimu wengi wako radhi kutembea na vyeti vyao makwapani na si kujitolea, ambapo kwa sasa Serikali imeelekeza nguvu zake katika kulipa madeni ya walimu. "Umetoka kuongelea hapa Shule ya Usese ina upungufu mkubwa wa Walimu, lakini kuna walimu huu ni mwaka wa nne yuko mtaani anatembea na cheti kwapani, hata ile kusema aende kujitolea na kuonesha uzalendo wake katika shule zenye uhitaji, lakini mimi niseme sasa kwanza Serikali inamalizia mzigo wa madeni ya walimu ya huko nyuma" amesema Dkt Avemaria. Aidha Dkt Avemaria ameongeza kuwa, "Mwalimu akikata tamaa ujue ni yule ambaye hajitambua, maana mwenye kujitambua anajua tunaenda wapi na ualimu ni harakat

Rais Magufuli akirudisha fomu ya kugombea Urais CCM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli, amerudisha fomu ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya Pili kupitia chama chake cha Mapinduzi (CCM), leo jijini Dodoma. Kushoto ni Katibu mkuu wa Chama cha mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ali akipokea fomu ya Mgombea wa urais.

RAO HEALTH TRAINING CENTRE RORYA YATANGAZA NAFASI ZA MASOMO

Image
MKUU WA CHUO CHA RAO HEALTH TRAINING CENTRE RORYA ANATANGAZA KUPOKEA MAOMBI KWA MWAKA WA MASOMO 2020/2021.  KATIKA KOZI ZIFUATAZO:  1. ORDINARY DIPLOMA IN CLINICAL MEDICINE (AFISA TABIBU) MIAKA 3 SIFA ZA MWOMBAJI: AWE NA UFAULU WA KIDATO CHA NNE KWA ANGALAU ALAMA 'D' IKIWEMO FIZIKIA'D' BIOLOJIA'D' KEMIA’D’ NA IKIWEMO HESABU NA ENGLISH NI KWA NYONGEZA KWA MASOMO MOJAWAPO.  2. CETIFICATE IN IN CLINICAL MEDICIN (AFISATABUBU MSAIDIZI) MIAKA MIWILI SIFA ZA MWOMBAJI: AWE NA UFAULU WA KIDATO CHA NNE KWA MASOMO ANGALAU ALAMA 'D' IKIWEMO MASOMO YA FIZIKIA'D' BIOLOJIA 'D' CHEMIA'D' NA IKIWEMO HESABU NA KINGEREZA KWA MASOMO MOJAWAPO FOMU ZINAPATIKANA CHUONI RAO MKOA WA MARA WILAYA YA RORYA AU KWENYE WEB SITE YETU  www.raocoop.org au wasiliana nasi kwa Email raohtc@raocoop.org au  0753624780 / 0758084663 / 0757862200 / 0763358409 / 0785191131/ 0784383329 WAHI SASA NAFASI NI CHACHE!!!!!! ALL COREESPONDENCES BE ADDRESS TO THE

Virusi vya corona: Raia wa mataifa 'salama' 14 ndio watakaoruhusiwa kuingia EU

Image
Umoja wa ulaya (EU) umetaja majina ya nchi 14 ambazo wananchi wake wanadaiwa kuwa salama kuruhusiwa kuingia katika nchi zake kuanzia Julai, mosi , licha ya mlipuko uliopo lakini Marekani, Brazil na China hazipo katika orodha hiyo. Mataifa yaliyotajwa ni pamoja na Australia, Canada, Japan, Morocco na South Korea. Muungano wa Ulaya upo tayari kuiongeza China katika orodha kama tu serikali yake China itatoa ruhusa sawa kwa wasafiri wa umoja wa ulaya, mwanadiplomasia anasema. Makatazo katika mipaka ya Umoja wa ulaya imeondolewa kwa wasafiri ambao ni raia wa Umoja wa ulaya kusafiri ndani ya ukanda wao. Sheria zilizowekwa dhidi ya wasafiri wa Uingereza ziko tofauti na makubaliano ya Brexit. Wananchi wa Uingereza wanachukuliwa sawa na raia wa Muungano wa Ulaya mpaka mwisho wa kipindi cha mpito Desemba, 31. Katika orodha ya sasa, maeneo salama ambayo yanaweza kuongezwa ni nchi za Algeria, Australia, Canada, Georgia, Japan, Montenegro, Morocco, New Zealand, Rwanda, Serbia, South K

YANGA yapania kulipa kisasi kwa KAGERA SUGAR

Image
KOCHA Mkuu wa Yanga,  Luc Eymael amesema kuwa anaamini wachezaji wake watalipa kisasi cha kufungwa mabao 3-0 na Kagera Sugar kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara walipokutana mara ya kwanza Uwanja wa Uhuru. Mchezo huo wa Ligi ulichezwa Januari 15,2020 ulikuwa ni wa kwanza kwa Eymael kukaa kwenye benchi la ufundi akichukua nafasi ya Mwinyi Zahera Akizungumza Eymael amesema kuwa ana waamini vijana wake watalipa kisasi kwenye mechi ya leo hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho ambalo ni muhimu kwao. "Walitufunga mchezo uliopita kwenye ligi ila sio huku kwenye Shirikisho, wachezaji wangu wapo vizuri na ninaamini watatumia nafasi ya kulipa kisasi ili kuendelea kulinda heshima ya uwezo wao," amesema. Mshindi wa mchezo wa leo atakutana na mshindi wa mchezo kati ya Simba na Azam FC hatua ya nusu fainali.

Sallam Kuukataa Mkono wa Harmonize Msibani, Chanzo ni hiki!

Image
MENEJA wa lebo ya muziki ya Wasafi Classic Baby (WCB),  Sallam Sk,   na msanii Harmonize ambaye aliwahi kuwa chini ya lebo hiyo, wameingia kwenye headlines baada ya Sallam kugoma kupokea mkono wa Harmonize katika msiba wa aliyekuwa mke wa Hamis Taletale (Babu Tale). Tukio hilo lililotokea msibani limeacha maswali mengi kwa baadhi ya watu walioshuhudia kitendo hicho, na kuhoji tatizo kati ya hawa ‘mabwana’ ni nini hasa mpaka kufikia Sallam kumwonyesha Harmonize chuki ya waziwazi mbele ya watu. Harmonize alisainiwa WCB, lebo ambayo inamilikiwa na msanii Diamond Platnumz  mwaka 2015 na kutambulishwa rasmi na ngoma ya ‘Aiyola’ ambayo ilifanya vizuri na kumweka kwenye ramani ya muziki wa Tanzania, Afrika na dunia kiujumla na baada ya hapo zikafuata ngoma nyingi ambazo zote zilifanya vizuri, chini ya usimamizi wa Lebo hiyo ambayo inasimamiwa na mameneja kadhaa akiwemo Sallam Sk, Babutale na Mkubwa Fela. Baada ya kudumu kwa takribani miaka minne yenye mafanikio katika lebo hiyo, Harmoni

TFF Yazipanga Yanga, Simba Usiku Kombe la FA

Image
Mechi  mbili za hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika zitakazohusisha timu za Yanga, Simba na Azam FC zitachezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini leo kuanzia saa 1.00 usiku. Kwa mujibu wa ratiba ya hatua hiyo iliyotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), mechi zote zitakazochezwa Uwanja wa Taifa zitafanyika usiku na zile za viwanja vingine zitachezwa kuanzia saa 10.00 jioni. Mchezo wa kwanza utakaochezwa usiku ni ule wa Yanga dhidi ya Kagera Sugar utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa leo kuanzia saa moja kamili usiku. Mechi hiyo itatanguliwa na ile ya Namungo FC dhidi ya Alliance ambayo imepangwa kuchezwa kuanzia saa 10.00 jioni kwenye Uwanja wa Kassim Majaliwa huko Ruangwa Lindi. Jumatano kutakuwa na mchezo mwingine baina ya Simba na Azam FC ambao nao utachezwa katika uwanja wa Taifa. Kabla ya mechi hiyo, mkoani Tanga kutakuwa na pambano baina ya wenyeji Sahare All Stars dhidi ya Ndanda FC utakaochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani. Ifahamike kwamba

Sugu ashindwa kujizuia amwaga chozi, akumbuka ya Gerezani,

Image
Aliekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini kupitia CHADEMA Joseph Mbilinyi ‘SUGU’ ameshindwa kujizuia baada ya kumkumbuka Mama yake Mzazi aliefariki kipindi yeye akiwa gerezani. Sugu alijikutana anamwaga machozi wakati akisimulia maisha yake alipokuwa gerezani na kifo cha Mama yake ambapo yeye alifichwa taarifa za kuumwa kwake.

EPL,EFL na PFA kuwapa nafasi makocha weusi (BAME)

Image
Ligi kuu ya soka England pamoja na kombe la ligi nchini humo (EFL) kwa kushirikiana na chama cha wachezaji wa kulipwa (PFA), wamekuja na mpango wa kuboresha uwezo kwa makocha weusi, wenye asili ya Asia na wanaotoka nchi nyingine ambazo hazijapiga hatua kwenye soka. Kwa mujibu wa kocha wa klabu ya Doncaster Rovers ambaye ni mshauri wa mpango maalumu wa watu weusi kwenye Premier League, Darren Moore amesema utaratibu huo utaanza msimu ujao wa 2020/2020. Utaratibu kamili wa mpango huo kwa msimu ujao ni kuwapa nafasi makocha sita wanaotoka kwenye nchi za (BAME), kujumuika kwenye benchi la ufundi msimu mzima kwenye vilabu kadhaa vinavyoshiriki kwenye Kombe la Ligi (EFL). Hadi sasa ni makocha 6 tu wanaotoka nchi za BAME ambao wanafundisha kama makocha wakuu katika vilabu 91 vya Premier League na EFL, hivyo lengo la mpango huo ni kuongeza idadi. VIGEZO NA MASHARTI Mpango huo ambao unafadhiliwa na Chama cha soka England (FA) pamoja na PFA, unamtaka kocha awe na leseni B ya ukocha

Jinsi wadukuzi walivyotapeli chuo kikuu Marekani $1.14m, Marekani

Image
Taasisi ya ngazi ya juu ya utafiti nchini Marekani inayofanyia kazi tiba ya ugonjwa wa corona imekiri kuwa iliwalipa matapeli dola milioni 1.14 sawa na (£910,000) kama kikombozi katika tukio ambalo lilishuhudiwa na BBC. Genge la majambazi la Netwalker lilivamia Chuo Kikuu cha California San Francisco (UCSF) Juni mosi 2020. Maafisa wa idara ya teknolojia walizima kompyuta zote za chuo hicho katika harakati za kuzuia kuenea kwa shambulio hilo la kimtandao. Chanzo cha habari ambacho hakikutaka kutajwa kiliifahamisha BBC na kuiwezesha kufuatilia majadiliano ya kikombozi katika njia ya moja kwa moja mtandaoni na wa wadukuzi hao. Wataalamu wa usalama wa mtandao wanasema majadiliano kama hayo sasa yanafanyika karibu kila sehemu duniani - wakati mwingine kinahusisha kiwango kikubwa cha fedha - kinyume na ushauri wa kisheria unaotolewa na mashirika ya upelelzi ikiwemo FBI, Europol na kituo cha kitaifa cha Uingereza kinachoshughulikia masuala ya usalama mtandaoni. Netwalker pekee ndi

CHADEMA Yatangaza Ratiba Kwa Wagombea wa Urais,na Ubunge

Image
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimefungua zoezi la uchukuaji fomu za kugombea Urais wa Tanzania, ubunge na udiwani, katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. Ratiba hiyo imetolewa Jumatatu tarehe 29 Juni 2020 na Reginald Munisi, Mkurugenzi wa Uchaguzi Chadema, wakati anazungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam. Munisi amesema, zoezi la uchukuaji na urejeshaji fomu ya urais wa Tanzania, litafanyika kuanzia tarehe 4 hadi 19 Julai 2020. Amesema katika mchakato wa kumpata mgombea Urais wa Tanzania ndani ya Chama, mtia nia au wakala wake Julai 4, mwaka huu Chama hicho kitafungua mlango wa mtia nia au wakala wake kuchukua fomu za kugombea urais wa Tanzania kupitia Chama hicho. Amesema fomu hizo za urais zitatolewa Makao Makuu ya Ofisi ya Chama hicho na kila mgombea atatakiwa kudhaminiwa na wanachama wasiopungua 100 kwa kila Kanda. “Tuna kanda 10 za CHADEMA Tanzania, nane zipo Bara na visiwani zipo kanda mbili, hivyo wago