Posts

Showing posts from August, 2019

MAGAZETI YA LEO 1/9/2019

Image

Dkt. Kigwangalla azindua kampeni ya 'Twenzetu Kutalii'

Image
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akizindua rasmi Kampeni ya “Twenzetu Kutalii” iliyoandaliwa na MISS Tanzania 2018, Queen Elizabeth Makune kuhamasisha Utalii wa ndani katika hoteli ya Serena, Dar es Salaam. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni hiyo, Dkt. Kigwangalla amewapongeza waandaaji wa tukio hilo kwa kuunga mkono juhudi za Serikali za kutangaza Utalii ndani na nje ya nchi. Amesema ipo haja ya viongozi na watu mashuhuri wakiwemo Wasanii kutumika kutangaza Utalii nchini. Amewataka wasanii wa Filamu waandae Filamu itakayoonesha na kubeba maudhui ya kuvitangaza Vivutio vya Utalii vilivyopo hapa nchini. Aidha, ameiagiza Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) iendelee kutoa ushirikiano kwa Balozi huyo wa Utalii  MISS Tanzania 2018/2019, Queen Elizabeth Makune kutokana na juhudi zake za kutangaza Utalii kwa vitendo.Pia ameiagiza TANAPA ianze kufanya mchakato wa kununua Meli mpya ya Kitalii itakayotumika Pwani ya Bahari ya Hindi.

Picha: Waziri Majaliwa azungumza na Waziri Mkuu wa Japan

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika kwenye hoteli ya The New Otani iliyopo Tokyo nchini Japan, Agosti 31, 2019 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amezungumza na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe.

Heshima na hadhi ya Tanzania yaendelea kunga’ra Kimataifa

Image
Heshima na hadhi ya Tanzania Kimataifa imeendelea kupanda kutokana na nia njema na kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo (Agosti 31, 2019) Jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa Serikali kwa mwezi Agosti 2019. Dkt. Abaasi anasema: “kwa mujibu wa Ripoti iliyotolewa Julai 12, 2019 kwa pamoja kati ya Transparency International na Afro-Barometer, Tanzania imeongoza katika nchi 35 kwa kuonesha juhudi za wazi katika kupambana na rushwa”. “Mafanikio haya yanatokana na msimamo thabiti wa Mhe. Rais Magufuli na Serikali yake katika kuimarisha taasisi muhimu kama vile TAKUKURU, Kuanzisha Mahakama ya Ufisadi na Uhujumu Uchumi, mfumo wa udhibiti wa rushwa katika manunuzi kupitia PPRA”, ameongeza Dkt. Abbasi. Akitolea mfano, amesema kuwa TAKUKURU

Waziri Biteko apiga marufuku shughuli za uchimbaji Madini ya Bauxite

Image
Waziri wa Madini, Doto Biteko kulia akimsikiliza kwa umakini Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mazinde Juu wakati wa mkutano huo. Waziri wa Madini Doto Biteko amepiga marufuku kuendelea kwa shughuli za uchimbaji wa madini ya Bauxite katika milima ya Bughai mpaka hapo utafiti wa athari za mazingira utakapofanyika. Marufuku hiyo ameitoa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Magamba wilayani Lushoto wakati wa ziara ya kutembelea eneo hilo na baadae kuzungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara. Amesema kuwa hakuna shughuli za uchimbaji zitakazofanyika mpaka hapo watakapoweza kupata majibu sahihi ya athari za kimazingira katika eneo hilo. “Nimepiga mafuruku shughuli zote za uchimbaji kuendelea kwani nimeona kuna mashine kule za uchimbaji hivyo ziondoeni “amesema Waziri huyo. “Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa wilaya naomba mlisimamie hili Lakini wakati tunaendelea kufanya hilo zoezi wale walikuwa na mashine pale lazima tujue ni wakina nani na wanapeleka wapi hiyo Bauxi

VIDE: BREAKING: Moto mkubwa umezukaka Jijini Arusha katika kiwanda cha nguo cha Sunflag

Image
Moto mkubwa umezuka katika Godauni la Kiwanda cha Nguo cha Sunflag Kilichopo Jijini Arusha ambapo mpaka sasa unaendelea kuteketekeza ambapo eneo hilo linahifadhiwa pamba ambapo Mkuu wa Wilaya tayari anashirikiana na wafanyakaz kuzima moto huo TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USIKOSE KU SUBSCRIBE

VIDEO: Msemaji mkuu wa serikali afunguka sakata la ndege Afrika kusini

Image
Serikali imewasilisha hoja tatu za nguvu katika mahakama ya Afrika Kusini, kuhusu zuio la ndege ya shirika la ATCL, pia amewatahadharisha watanzania wanaoihujumu serikali kwenye hili swala la ndege kuzuiwa na kusema watafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USIKOSEW KU SUBSCRIBE

Shehena feki la vipodozi yadakwa

Image
Jeshi la polisi mkoani Pwani, linamshikilia  Albert Kiwia (45) mkazi wa Kimara Dar es salaam kwa kosa la kusafirisha shehena ya vipodozi feki mbalimbali  ,kwa kutumia gari aina ya Toyota Nissan. Katika hatua nyingine, Jeshi hilo limefanikiwa kukamata madumu saba ya mafuta ya diezel yakiwa na ujazo wa lita 20 kila moja mali inayodhaniwa kuwa ni ya wizi. Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa aliwaambia waandishi wa habari kuwa ,mtuhumiwa huyo amekamatwa agost 29 mwaka huu, katika eneo la Mizani ya zamani -Kibaha Mji. Alifafanua, licha ya tuhuma hiyo ya kusafirisha vipodozi hivyo ,jeshi hilo likamtaka aonyeshe kwa TRA stakabadhi alizolipia ushuru katika mipaka ya nchi wakati akiingiza vipodozi na hakuwa navyo Aliwataka ,wafanyabiashara wenye tabia ya kuingiza bidhaa zao nchini kwa kukwepa kulipa kodi ,kuacha mara moja . Wankyo alisema ,wamedhibiti mianya yote kwa wale wanaojaribu kukwepa kulipa kodi katika barabara zote za mkoa na wale watakaokamatwa hatua kali za kis

Picha: Spika Ndugai aongoza kikao cha Kamati ya Bodi ya Uwekezaji Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola

Image
Spika, Job Ndugai aongoza kikao cha Kamati ya Bodi ya Uwekezaji Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Mjini Zanzibar. Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akiongoza kikao cha kamati ya Bodi ya uwekezaji wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (hawapo kwenye picha) katika hoteli ya Madinat Al Bahr Business and Spa Mjini Zanzibar, katika Mkutano wa 50 wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika ulioanza leo tarehe 30 Agosti, 2019 mpaka tarehe 5 Septemba, 2019

Serikali yafuta miliki ya mashamba ya MOA, kisa?

Image
Serikali imefuta miliki ya Mashamba matatu ya Mkomazi Plantantions maarufu MOA yaliyopo wilaya ya Mkinga mkoani Tanga kutokana na kukiuka masharti ya uendelezaji ikiwemo kutelekezwa bila kufanyiwa maendelezo yaliyokusudiwa  na kutolipiwa kodi ya pango la ardhi. Uamuzi huo umetangazwa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alipozungumza na wananchi wa Mayomboni wilayani Mkinga mkoani Tanga alipokwenda kutatua mgogoro wa muda mrefu katika eneo hilo. Mashamba yaliyofutiwa ni lenye hati Na 9780  na ukubwa wa ekari 14,688, shamba  Na 4268  ekari 804 na Shamba lenye Hati Na 9781  ekari 246 ambapo mashamba yote matatu yana ukubwa wa ekari 15,738. Kufuatia uamuzi huo, jumla ya vijiji kumi vyenye kaya 3,236 zilizo na wakazi 16,450 zitanufaika na uamuzi wa serikali kutokana na wananchi wake kuvamia mashamba hayo na kufanya maendelezo ya kujenga makazi, shule pamoja na kuendesha shughuli za kilimo cha mazao ya kudumu na ya muda mfupi. Vijiji vilivyonufaika ni

Alichokiongea Jaji Kiongozi na Wataalamu kutoka Benki ya Dunia, hiki hapa

Image
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Dkt, Eliezer Feleshi, amefanya mazungumzo na wadau kutoka Benki ya Dunia(WB) juu ya tathmini ya  Mradi wa Maboresho ya Mahakama ya Tanzania  yanayofanywa chini, ambapo umeleta matokeo chanya katika shughuli za Mahakama.  Akizungumza  na ujumbe wa benki hiyo, katika ofisi za  Mahakama Kuu ya Tanzania, Jaji Kiongozi  alisema  mradi huo, umeweza kusaidia kuboresha shughuli za utendaji kazi wa Mahakama na kusogeza huduma karibu na wananchi. “Tumeweza kusikiliza kesi kwa kutumia Mahakama Inayotembea (Mobile Court) jijini Mwanza, hivyo ni moja ya maboresho ya huduma za Mahakama, yaliyotokana na mradi huu,” alisema  Jaji Kiongozi.  Aliongeza kuwa mradi huo unaofadhiliwa kwa fedha za mkopo kutoka benki hiyo,  umewezesha  Mahakama ya Tanzania,kusikiliza kesi kwa njia ya Mtandao ‘Video coference’, ambapo, ugeni huo, ulitaka kufahamu tathimini ya eneo hilo, alisema  umeweza kutumika   katika baadhi ya mikoa,ambayo ni  Mbeya, Bukoba, na Kituo cha

Waziri Bashungwa atishia kujiuzulu TBS isipobadilika

Image
Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa ametishia kujiuzulu iwapo Shirika la Viwango nchini (TBS) halitabadili mwenendo wake katika kushughulikia kero na malalamiko ya wafanyabiashara. Bachungwa aliyasema hayo mjini Makambako Mkoani Njombe wakati alipokutana na wafanyabiashara kutoka mikoa saba nchini kujadili changamoto zinazoikabili sekta ya biashara. Katika mkutano huo uliotoka na maazimio ya kuiomba serikali kupunguza utitiri wa kodi, tozo na leseni kwa wafanyabiashara ili kunusuru sekta hiyo pia waziri huyo kwa mara nyingine tena aliinyooshea kidole TBS. "TBS nimeshawaambia kwamba nitajiudhuru uwaziri kama hamtabadilika sasa kwa umri huu na haka kakibarua nataka nifanye vizuri." "TBS ujumbe ndio huo nataka tushirikiane kuhakikisha utitiri wa kero zilizokuwepo zisizokuwa na lazima zinakwisha, ifike mahali basi hawa wakawe mashahidi kwamba kweli TBS mmebadilika," alisema. Aliitaka TBS kubadilika ili kuendana na kasi ya serikali katika kushug

Pacha wa Kagera waliokuwa wameungana warejea Tanzania baada ya kutenganishwa

Image
Pacha waliougana Anisia na Melnes Bernard,  wamewasili katika uwanja wa ndege wa Julius  Nyerere jijini Dar es salaam  wakitokea nchini  Saudi Arabia baada ya kutenganishwa, matibabu yaliyogharimu dola za Marekani 500,000 (zaidi ya Sh bilioni 1.1) Mapacha hao walikuwa wameungana kifua, tumbo na nyonga walianza kufanyiwa upasuaji wa kutenganishwa Disemba 23 katika hospitali ya King Abdallah. Baada ya kutenganishwa, pacha hao ambao walizaliwa wakiwa na miguu mitatu, sasa kila mmoja amebaki na mmguu mmoja. Wakizungumza wakati walipowasili, madaktari bingwa wa upasuaji kwa watoto walisema waliungana na madaktari 35 wa Saudi Arabia na nchi zingine  ili kufanikisha upasuaji huo ambao ulifanyika ndani ya sasa 14. Mmoja wa Madaktari hao Dk Petronia Ngiroi, alisema madktari bingwa wa sehemu mbalimbali wa watoto walifanya uchunguzi na kuhakikisha kuwa upasuaji huo utafanikiwa. “Tangu wakiwa Muhimbili tuliwafanyia vipimo na tukawasiliana na madktari wa Saudi Arabia na tukawatumia vipi

UVCCM watoa pongezi kwa Rais Magufuli

Image
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Katavi umempongeza Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa utekelezaji wa miradi mikubwa mkoani Katavi. Akitoa pongezi hizo Katibu wa UVCCM Mkoa, Bw. Theonas Kinyonto amesema ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mpanda hadi Tabora unaashiria utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho ya mwaka 2015/20. Aidha kupitia mradi wa uboreshaji miji utekelezaji wa mradi wa barabara ya lami ya kilometa 7.7 katika manispaa ya Mpanda uliogharimu shilingi bilioni 8 ambao kwa sasa umekamilika kwa asilimi 97 Pia wamemsukuru Rais kwa kutoa fedha za kujenga kituo kikubwa cha mabasi halikadhalika kuboresha miundombinu ya afya katika mkoa wa Katavi sanjari na ujenzi wa Hospitali za Wilaya tatu katika mkoa wa Katavi Katika hatua nyingine, Bw. Kinyonto ametoa wito kwa Vijana kujiunga katika makundi ili kupata mikopo ya Halamshauri ambapo jumla ya shilingi milioni 700 zimetengwa kwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya kuwezesha makundi mbalimbali Pia ameponge

VIDEO: Madiwani wa CHADEMA wasusia uchaguzi watoka nje

Image
Madiwani wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA wilayani Biharamulo mkoani Kagera wamesusia uchaguzi wa kamati za kudumu za balaza la madiwani wakidai kuwa hawakutendewa haki katika uchaguzi huo TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USIKOSE KU SUBSCRIBE

VIDEO: Fahamu sheria na haki za wanawake waliochika

Image
Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 imefafanuliwa na mwanasheria wa kituo cha sheria na haki za binadamu Arusha Freddy Lymo ambapo amesema wanawake wengi wananyanyasiki kutokana na kutofahamu haki zao katika ndoa TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USIKOSE KU SUBSCRIBE

Kupatiwa chakula mashuleni, Kiwango cha ufaulu chaongezeka

Image
Na. Clavery Christian Kagera Halmashauri ya wilaya Biharamulo mkoani Kagera imefanikiwa kwa kiwango kikubwa kuongeza ufaulu wa wanafunzi wa madarasa ya awali, darasa la nne, na darasa la saba baada ya kuanza kuwapatia huduma ya uji na chakula mashuleni. Hayo yamesemwa na mh,  Samweli Kalimanzira mwenyekiti wa kamati ya elimu, maji na afya katika kikao cha robo ya nne ya mwaka cha balaza la madiwani wilayani humo ambapo amesema kuwa ufaulu wa wanafunzi mashuleni umeongezeka kutokana na shule nyingi za wilaya hiyo kuanza kutekeleza maamuzi ya kamati hiyo ya kuwapatia uji na chakula wanafinzi mashuleni ili kuwaondolea hali ya kuwa darasani wanawaza wataondoka saa ngapi kwenda nyumbani kula kutokana na njaa wanayokuwa nayo. Kamati hiyo imeshauri kuwa shule kumi (10) ambazo zimebaki bila kuwa na huduma ya uji wala chakula shuleni wazazi na walezi waendelee kuhamasishwa na watumishi wakishirikiana na madiwani ili shule hizo ziweze kutoa huduma hiyo kwa wanafunzi bila kuchelewa. Aidh

Mgonjwa wa miaka 101 awekewa kifaa Maalum cha kurekebisha mapigo ya moyo JKCI

Image
Kwa mara ya kwanza madaktari bingwa  wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wamwekea mgonjwa mwenye umri wa miaka 101 kifaa maalum cha kurekebisha  mapigo ya moyo ili yawe sawa (kwa jina la kitaalamu Pacemaker). Kifaa hicho kisaidizi cha moyo huwekewa wagonjwa ambao mapigo yao ya moyo yako chini ya asilimi 30 kwa dakika. Akizungumza baada ya kumfanyia upasuaji mdogo na kumwekea mgonjwa kifaa hicho  Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa JKCI Yona Gandye alisema mara nyingi  wanawawekea kifaa hicho  wagonjwa wenye umri wa miaka 80 kushuka chini lakini leo hii wamevunja rekodi na  na kuweka kwa mgonjwa wa umri wa  miaka 101. “Kabla ya kufanya upasuaji tulimfanyia mgonjwa uchunguzi wa kina na kugundua  mfumo wake wa umeme wa moyo unahitilafu na mapigo ya moyo yapo chini ya asilimia 20 hivyo tumemuwekea kifaa ambacho kitausaidia moyo kuongeza mapigo yake na mara baada ya kumwekea kifaa hiki  mapigo yake ya moyo yako vizuri kati ya asilimia 60 na 100 kwa dakik

Vijana washauri kupima DNA kabla ya kuoana

Image
Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dk Elineema Meda, amewashauri vijana kupima vinasaba (DNA) kabla ya kuona ili kuepuka kupata watoto wenye ugonjwa wa selimundu. Akizungumza, Dk Meda alisema ni vema vijana kupima ili kujua kama wanachembechembe za selimundu kwani itasaidia kupunguza kasi ya ugonjwa huo. “Ugonjwa huu wa selimundu unatokea pale ambapo wazazi wote wawili watakuwa  DNA yenye chembechembe za selimundu, hapa ndio kunauwezekano wa wazazi kuzaa watoto wenye ugonjwa huo au hata kama hawana watakuwa na chembechembe za selimundu. “Kasi ya ugonjwa wa selimundu imeongezeka katika bara la Afrika lakini ninachosema ni kuwa ugonjwa huu unaepukika kama vijana au wazazi watakapoamua kupima DNA kabla ya kuoana kwani wakishajua wanaweza kufanaya maamuzi ya kuchagua,”alieleza Dk Meda. Kwa mujibu wa Dk Meda alisema utafiti uliofanywa na Muhimbili unaonesha kati ya watu 100 waliofanyiwa vipimo, 13 wanachembechembe za selimundu. Alisema iki

Makamu Mwenyekiti mpya apatikana Halmashauri ya Hai

Image
Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Mkoani Kilimanjaro, limefanya uchaguzi na kumchagua, Elingaya Massawe kuwa Makamu Mwenyekiti wa halmashauri hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja. Baraza hilo limefanya uchaguzi huo Ijumaa hii, chini ya usimamizi wa Mwenyekiti wake Helga Mchomvu. Massawe aliibuka mshindi baada ya kupata kura 15 kati ya 22 zilizopigwa na kumshinda mshindani wake Deo Kimaro ambaye alipata kura saba.

Watumishi wa Mahakama ya Tanzania wapewa darasa

Image
Watumishi wa Mahakama ya Tanzania watakaofanya kazi katika Mahakama Inayootembea ‘Mobile Court’ katika jijini la Dar es Salaam, wametakiwa kuwa tayari kufanya kazi katika  mazingira mapya ya Mahakama hiyo, ili kutoa huduma bora za  kimahakama. Akizungumza katika ukumbi wa kufanyia mikutano Kitengo cha Maboresho ya Huduma  za Mahakama ya Tanzania (JDU) , Mtaalam kutoka Benki ya Dunia (WB),Waleed Malik amewataka watumishi hao kufanya kazi kwa ushirikiano bila  kujali nyadhifa za utumishi wao,  Aidha  ameongeza kwa kusema kuwa si mtu mmoja atakaye husika katika utendaji kazi wa Mahakama hiyo , bali jopo la watumishi , ambapo aliwataja baadhi yao akiwemo Hakimu Mkazi Mfawidhi, Karani, Afisa Habari, Katibu Mahususi, Mtaalam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Dereva. “Mnatakiwa kuwa tayari kupata taarifa za ghafla ambazo zitawataka kufanya maboresho katika utendaji kazi wenu, na namna ya kutatua matatizo ya ghafla yanayotokea katika vifaa vinavyotumika kufanyia kazi ndani ya Mah

TACAIDS yajidhatiti kuzuia maambukizi mapya ya VVU

Image
Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) imejidhatiti kukabiliana na maambukizi mapya ya ugonjwa huo kwa kuanzisha vituo vya kutoa huduma za ushauri nasaha na upimaji katika maeneo yote ya barabara kuu za kwenda nchi jirani. Akizungumza katika kipindi cha “TUNATEKELEAZA” Mkurugenzi Mtendaji wa Tume hiyo Dkt. Leonard Maboko amesema mpaka sasa vituo 20 vimeanza kutoa huduma katika barabara kuu za kuelekea nchi jirani ili kuyafikia makundi maalum kama madereva na vijana wanaoishi katika maeneo ambayo yana mikusanyiko mikubwa ya watu kutokana na shughuli za kibiashara. “Katika mradi huu bilioni 12 zimetumika katika kuanzisha vituo hivyo 20 ambapo matarajio yetu katika mwaka 2019/20 tutaanzisha vituo vingine 20 kwa lengo la kuhakikisha tunayafikia makundi maalum kama wavuvi, vijana  wa kiume na kike,” alisisitiza Dkt.  Maboko Akifafanua Dkt. Maboko amesema kuwa Tume hiyo itaendelea kuchukua jitihada za makusudi katika kuzuia maambukuzi mapya na kuhakikisha wale walioathirika wana

BREAKING NEWS: Watu watano wafariki baada ya magari kugongana, moja lawaka moto

Image
Watu watano wamefariki baada ya gari la Dangote lililokuwa limebeba malighafi ya kutengenezea saruji likielekea Mtwara kugongana na Gari dogo na kupinduka kisha kuwaka moto baada ya kupoteza muelekeo na kugonga nguzo ya umeme rufiji mkoani Pwani. RPC Rufiji,  Onesmo Lyanga amethibitisha taarifa hizo. Endelea kufuatilia Muungwana Blog kwa taarifa zaidi.

MAGAZETI YA LEO 31/8/2019

Image