Posts

Showing posts from June, 2019

Tetesi: Muda wowote Simba SC kumtangaza Ibrahim Ajibu kama mchezaji wao

Image
Inaripotiwa kuwa kuanzia leo Ibrahim Ajibu Migomba ni mchezaji halali wa Simba SC ambapo mkataba wake na Yanga SC umemalizika rasmi jana. Taarifa zinaeleza kuwa Simba SC ilikuwa inasubiria kumtangaza mchezaji huyo mara baada ya mkataba wake na Yanga SC kumalizika.

RITA yazitaka bodi za wadhamini kufanya marejesho

Image
Serikali kupitia Wakala wa Usajili, Udhamini na Ufilisi (RITA), imezitaka Bodi mbalimbali za wadhamini kufanya marejesho kwa mujibu wa sheria ya muunganisho wa wadhamini kwa muda sahihi kila mwaka. Bodi hizo za wadhamini ni pamoja na vyama vya siasa, taasisi mbalimbali zisizo za serikali (NGOs), taasisi za kuabudu zikiwamo makanisa, vilabu vya mpira wa miguu na nyinginezo. Hayo yamesemwa jana na Wakili wa Serikali  Mwandamizi, Edna Kamara, katika viwanja vya maonesho sabasaba ambapo amesema bodi nyingi zinafanya vizuri lakini zipo ambazo zinasuasua hivyo kuepuka sheria kuchukua mkondo wake wafanye marejesho haraka iwezekanavyo. “Bodi ya wadhamini inatakiwa kufanya marejesho kila mwaka tarehe husika kwa kujaza fomu namba T.1.5  na kulipia ada ya Sh, 50000 kwa mujibu wa sheria ya muunganisho sura ya 318 toleo 2002 kuepuka kulipa faini. “Hapa sabasaba huduma hizo zipo zinaendelea kwa wanaoona uvivu kufika katika ofisi za RITA wafike hapa tuwahudumie haraka,” amesema Edna. Aidh

RC Ayoub azitaka Mamlaka za bima kusambaza elimu kwa jamii

Image
Na Thabit Hamidu,Zanzibar Uongozi wa mamlaka ya Bima Tanzania umetakiwa kutoa elimu kwa jamii kukata na kutumia bima kutoka kwa watoa huduma waliosajiliwa na mamlaka husika ili kuongeza pato la taifa pamoja na kudibiti watu waoghushi huduma hiyo. Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud ametoa wito huo wakati akiungungumza na viongozi ,wadau na wananchi katika maadhimisho ya siku ya bima Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya kumbukumbu kisonge mjini unguja. Alisema endapo makampuni na wataalamu wa bima watakuwa na utamaduni wa kutoa elimu ya mara kwa mara wananchi watapata uelewa juu ya umuhimu wa huduma Bima na  hawatasita kununua huduma hiyo. "Kwa sababu mamlaka ya bima ni chombo cha ushauri kwa serikali kuhusu masuala ya soko la bima,ni matumaini yangu wananchi sasa watanunua huduma za bima,na endapo kutatokea migogoro au kutoelewana kati ya kampuni ya bima na mteja ninauhakika mamlaka yenu itakuwa tayari kulitatua na kulipatia ufumbuzi"alisema Ayo

Watu 228 wafariki Australia kwa homa

Image
Takribani watu 228 wameripotiwa kufariki nchini Australia kutokana na homa ya mafua huku wengine 100,000 wakiuguza virusi hivyo, idadi kubwa ikilinganishwa na mwaka wa 2018 ambapo vifo 58,824 viliripotiwa. Mkuu wa afya nchini humo amesema virusi hivyo vimeendelea kusambaa licha ya chanjo iliyotolewa kwa zaidi ya watu milioni 11 na kuongeza kuwa taifa hilo linapitia wakati mgumu kutokana na msimu wa baridi na wanatarajia hali hiyo kuboreka kati ya mwezi wa Julai na Septemba.

Waziri Bashungwa awajia juu wanaobeza ubora wa Korosho

Image
Waziri wa Viwanda na Biashara ,Innocent Bashungwa amekemea baadhi ya Watanzania wanaopotosha  na kukandia kuwa korosho ya Tanzania iliyopo kwenye maghala ,haina ubora ambapo amewapasha kuacha propaganda zisizo na tija kwa Taifa. Aidha ameielekeza DAWASA na TANESCO kukimbilia fursa ya kutoa huduma ya maji na umeme kwa wawekezaji pasipo kuwakwamisha huduma hizi ili wazalishe zaidi na serikali ipate mapato makubwa. Akitembelea kiwanda cha korosho Terra cashew kilichopo ,Tanita wilayani Kibaha mkoani Pwani, Bashungwa alieleza watu hao hawalitakii mema Taifa. Aliweka bayana kwamba, tayari kwa sasa kuna korosho ya kutosha na yenye ubora katika maghala 37 nchini . “Nchi yetu inategemea zao hili la kibiashara wakitokea watu wapotoshaji inakuwa haileti maana na kushusha sifa ya nchi katika biashara ya zao hilo”. “Nilitembelea maghala hayo na wataalamu wangu, tumejiridhisha ,korosho yetu ni nzuri kwa grade ya I na ya II na ipo katika thamani”alisisitiza Bashungwa. Akizungumzia sual

Simba SC wapatwa na msiba

Image
Uongozi wa Simba SC umeeleza kuguswa na kifo cha Mwenyekiti wa Tawi la Simba Damu Fans (SDF), Alfred Kehongo.

Walimu wa masomo ya Hisabati na Sayansi kukuza ufaulu nchini

Image
Walimu wa masomo ya  Hisabati  na Sayansi nchini wametajwa kuwa chachu ya kuendelea kukuza kiwango cha ufaulu katika masomo hayo na hivyo kuchochea ujenzi wa dhana ya uchumi wa viwanda. Akizungumza wakati akifungua mkutano wa mwaka wa chama cha walimu wa Hisabati na Sayansi   Jijini Dodoma Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Sera Uratibu na Uwekezaji) Bi Dorothy Mwaluko amesema kuwa walimu wa masomo hayo wamekuwa wakifanya kazi kubwa yakuwaandaa vyema wanafunzi wanaochukua michepuo ya sayansi na hivyo kuchochea ufaulu kuongezeka. “ Nawapongeza na kuwataka muongeze juhudi katika kuhakikisha kuwa tunasaidia katika ujenzi wa uchumi wa viwanda kwani unategekea wataalamu wa Hisabati na Sayansi ili azma hii ya Serikali ya Awamu ya Tano iweze kutimia kwa wakati” Alisisitiza Bi Mwaluko. Akifafanua amesema kuwa walimu wa masomo hayo wamekuwa wakijitoa kwa dhati kutekeleza majukumu yao ili kuwawezesha wanafunzi wengi zaidi kupenda masomo ya Sayansi na Hisabati na hatimaye

Serikali yashirikiana na Kampuni za simu kusaidia watoto na Wanawake

Image
Serikali imesema itaendelea kushirikiana na kampuni za simu ili kuwasaidia wananchi katika mambo mbalimbali ya kijamii yakiwemo ya Afya, Elimu  na Miundombinu. Akizungumza  katika hafla ya uzinduzi wa Vodacom Tanzania Foundation, Naibu  Waziri wa  Tamisemi,  Joseph Kandege amesema Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ili kuwawezesha Vodacom kuwafikia watanzania wote wenye mahitaji .  Waziri kandege Amesema Vodacom wanafanya kazi ambazo zinagusa jamii kama afya   na kuwasaidia watoto wa kike kwenda shule kwa kuwapatia vitaulo vya kujihifadhia katika hedhi, pia wameendelea kuwasaidia kina mama juu ya ugonjwa wa fistula ambayo inawapelekea wamama wengi kutengwa na jamii. “ Serikali itahakikisha inaimarisha miundombinu ili kuhakikisha vodacom inawafikia  watu wenye uhitaji na pia tumeona jinsi walivyoweza kuwasaidia watoto wa kike na wakinamama wenye fistula juu ya kupata matibabu  ya ugonjwa huo na kugawa vitaulo kwa watoto wa kike wenye uhitaji, ambao wanakosa kwenda shule

MAGAZETI YA LEO 1/7/2019

Image

Maelfu ya Watanzania wamuombea Rais Magufuli

Image
Na  Ferdinand Shayo,Arusha. Maelfu ya Watanzania wamefanya maombi ya kumuombea Rais wa Tanzania Dr.John Pombe Magufuli pamoja na Viongozi wa serikali ili kuendeleza nguvu katika ujenzi wa Tanzania mpya ili kufukia uchumi wa Viwanda kama ilivyo ndoto ya Rais. Mji wa Arusha umefurika maelfu ya watu kutoka ndani na nje ya mkoa wa Arusha pamoja na mikoa ya Kilimanjaro,Manyara,Singida,Dodoma ambao wamekusanyika kwa ajili ya kuiombea serikali  na Watanzania kwa ujumla. Mkurugenzi Msaidizi wa Redio  Safina ,Hellen Lema amesema kuwa maombi hayo yanalenga kuomba Mungu azidi kumpa nguvu Rais Magufuli ili aweze kuwatumikia vyema Watanzania  na taifa la Tanzania lizidi kubarikiwa na kusonga mbele kiuchumi. Mchungaji Pascal Thomas  amesema kuwa maombi hayo ya toba  dhidi ya maovu mbalimbali na kuhamasisha watu kumcha Mungu na kuondokana na uovu pamoja na kuwaombea viongozi. Kwa upande wao wananchi Ester Mremi na  Joel Molel walioshiriki katika maombi hayo wameeleza umuhimu wa kuliom

KMC yazidi kusajili yachukua mwingine kutoka Ndanda FC

Image
 Mshambuliaji Vitalisy Mayanga amejiunga na klabu ya KMC  kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea Ndanda FC. KMC inaendelea kujiimarisha kwenye usajili ili kupambana kwenye msimu ujao.

Singida United yasajili mshambuliaji kutoka Ghana

Image
Klabu ya Singida United FC imeanza rasmi usajili wake kuelekea msimu ujao kwa kumnasa mshambuliaji Herman Frimpong kutoka nchini Ghana akisaini mkataba wa miaka mitatu. Frimpong mwenye umri wa miaka 22 ameshatua nchini Tanzania na amekabidhiwa jezi namba 14.

Mtambo wa Megawati 300 kutengenezwa Mtwara

Image
Na Omary Mngindo, Mkuranga SERIKALI imeeleza kuwa ina mpango wa kutengeneza mtambo mkubwa utaozalisha Megawati 300 za umeme, kisha kuusafirisha kutoka mkoani Mtwara kwenda Kinyerezi jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu ameyasema hayo alipozungumza na wananchi wa Kijiji cha Njopeka, Kata ya Mjawa wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani, akiwa kijijini hapo mwishoni mwa wiki, ambapo alisema hatua hiyo inalenga kuboresha huduma ya umeme. Aidha alisema kuwa serikali imefanya tathmini ya fidia kwa wananchi wa maeneo ya Rufiji, Mkuranga na Dar es Salaam ambao wamepitiwa na bomba la gesi na nguzo za umeme, huku akiombaradhi kuchelewa kulipwa fidia, na kwamba zoezi hilo linataraji kuanza Julai mwaka huu. "Malipo yataanza mwezi Julai kwa wakazi waishio Mkoa wa Dar es Salaam, baada ya hapo zoezi litaendelea tena kuanzia mwezi wa nane mpaka wa kumi na mbili mwaka huu kwa wakazi wa maeneo ya Mkuranga, niwaomberadhi kwa kuchelewa fidia hizo" alisema Mgalu. Aidh

VIDEO: Chadema waahidi kuchukua maamuzi haya ya kisiasa kuhusu Lissu kufutwa Ubunge

Image
Baada ya aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu kutangazwa kufutwa Ubunge na Spika Job Ndugai, Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt. Vicent Mashinji amefunguka maamuzi ya kisisasa ambayowamepanga kuyachukua. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI....USISAHAU KUSUBSCRIBE

LIVE: TAMKO LA CHADEMA BAADA YA TUNDU LISSU KUVULIWA UBUNGE NA SPIKA NDUGAI (+VIDEO)

Image
Chadema watoa tamko lao baada ya hivi juzi Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai kutangaza kuvuliwa ubunge aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI....USISAHAU KUSUBSCRIBE

Singida United yamsajili Marcelo

Image
Beki wa kushoto kutoka Malindi FC ya Zanzibar Muharami Salum Marcelo ametua Singida United kwa mkataba wa miaka mitatu. Marcelo mwenye umri wa miaka 24 ana uwezo pia wa kucheza kama winga wa kushoto.