Posts

Showing posts from January, 2020

Simba kuvaana na Costal Union leo

Image
Timu ya soka ya  Simba kuoneshaana ubabe na Costal Union leo ambao mchezo utachezwa  kwenye Uwanja wa Uhuru ukiwa ni mchezo wa ligi kuu. Simba kwa sasa wako nafasi ya kwanza wakiwa na pointi 44 baada ya kucheza mechi 17, Coastal Union wenyewe wapo nafasi ya tatu na alama zao 30, wamecheza mechi 17 kama wapinzani wao. Sasa rekodi zinaonyesha kuwa kwa msimu uliopita wa 2018/19 ambao Coastal Union ilipanda daraja, iliambulia kichapo mechi zake zote mbele ya Simba jambo linaloufanya mchezo wa leo kuwa mgumu.

Waliofariki kwa virusi vya Corona nchini China wafikia 213

Image
Idaadi ya watu waliofarki kufuatia  wimbi la virusi vya Corona nchini China yaripotiwa kuongezeka na kufikia watu  213. Wizara ya afya ya China imetangaza kwamba watu  213  wamefariki huku wengine 9692 tayari wameambukizwa virusi hivyo. Miongoni mwa waathirika wa virusi hivyo1527 wapo katika hali maututi.

TFF yawaka juu ya upotoshaji wa ratiba ya ligi kuu

Image
Taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuhusiana na upotoshwaji wa Ratiba ya Ligi Kuu Bara kwa mechi za Yanga.

China yaagiza 'mask' milioni 200 kutoka Uturuki

Image
Kutokana na kuibuka kwa mlipuko wa aina mpya ya virusi vya Corona (2019-nVoC), uihitaji wa visetiri vya mdomo na pua“mask” umeongezeka. Mamlaka nchini China zimefahamisha kwamba katika siku 10 za hivi karibuni wameagiza mask milioni 200 kutoka  mashirika ya kitabibu ya Uturuki. Moja ya hatua muhimu ya kujikinga na virusi hivyo vya Korona ni kwa kutumia mask. Pamoja na kwamba China ni moja ya wazalishaji wakubwa wa mask duniani kuibuka kwa mlipuko wa virusi vya Korona kumepelekea kushindwa kutosheleza mahitaji yake ya ndani. 

Tanzania yapigwa marufuku bahati nasibu ya viza Marekani

Image
Serikali ya Marekani imepiga marufuku raia wa Tanzania kushiriki katika bahati nasibu wa kupata viza ya kuingia Marekani. Bahati nasibu hiyo hutoa viza kwa watu takribani 50,000 kutoka nchi zenye kasi ndogo ya maendeleo kila mwaka kuingia na kufanya kazi Marekani. Nchi ya Sudani pia raia wake wamepigwa marufuku kuingia katika bahati nasibu hiyo. Wakati huo huo raia wa nchi nne ikiwemo mbili za Afrika Nigeria na Eritrea wamepigwa marufuku kabisa kuomba viza za kuhamia Marekani. Hata hivyo raia wa nchi hizo ambao watataka kuingia Marekani kwa kutalii ama biashara wataruhusiwa. Wiki iliyopita, vyombo vya habari vya Marekani viliripoti juu ya rasimu ya marufuku mpya ya kuingia Marekani kwa mataifa saba. Ni taifa moja tu la Belarus ambalo lilitajwa katika rasimu ya awali ambalo halijaorodheshwa katika taarifa za leo. Afisa wa ngazi ya juu nchini Marekani amesema kuwa nchi hizo sita zimeshindwa kufikia "kiwango stahiki cha ulinzi na kupashana taarifa". "Nchi

Afumwa akichimba mchanga wa kaburini

Image
Wananchi wa Mtaa wa Fadhili Bucha Kata ya Buhalahala Halmashauri ya Mji wa Geita, wamekumbwa na taharuki, baada ya kumkamata mwanamke mmoja, Mariam Kaijage akichimba mchanga na kuchuma majani yaliyoota juu ya Kaburi walilozika mmoja wa wanafamilia wa mtaa huo. Mwanafamilia huyo aliyejulikana kwa jina la Abel Njige aliyezalizikwa Desemba 24, 2015 ndilo ambalo limechimbwa mchanga na mwanamke huyo kama ilivyoelezwa na mdogo wa marehemu. Amesema kuwa kifo  cha ndugu yake kilitokea ghafla siku chache baada ya kupatwa na maradhi ya akili, akiwa na hofu huenda anayetafutwa hivi sasa ni yeye. Akiongea na EATV/EA Radio katika eneo la tukio, mtuhumiwa huyo ambaye awali alishikiliwa katika ofisi ya mtaa wa Fadhili Bucha kwa mahojiano zaidi kabla ya kuachiwa huru amesema mchanga huo ulikuwa ni tiba ya mwanaye anayesumbuliwa na maradhi ya miguu kwa muda mrefu. Hata hivyo Doto anashangazwa na uongozi wa mtaa huo kumwachia huru mwanamke huyo kabla hajaeleza kwa kina lengo la yeye kufanya hivyo

MAGAZETI YA LEO 1/2/2020

Image

Yanga, GSM watoa msaada

Image
KLABU ya Yanga kupitia kwa mdhamini wao Kampuni ya GSM leo Januari 30, 2019 wamefanikisha kutoa masaada wa fedha mahitaji ya chakula cha miezi mitatu pamoja na kugharimia matibabu ya Anna Majaliwa. Yanga imetoa msaada huo kwenye familia ya Anna ambaye anasumbuliwa na tatizo la mwili kukosa fahamu ndani ya miaka mitatu jambo lililompelekea kushindwa kupata choo kwa zaidi ya miezi sita. Akizungumza Anna amesema kuwa alipatabtatizo hilo kwa zaidi ya miaka hiyo mitatu jambo linalomfanya kupata tabu kila kukicha hivyo anawashukuru sana Yanga kupitia mdhamini wao GSM kwa kutambua tatizo lake. “Najisiki faraja sana kuiona timu yangu Yanga kupitia kwa mdhamini GSM, ambao kwa namna kubwa wametambua tatizo langu na kujitolea msada huu wa chakula pamoja na godoro ambalo kiukweli sikuwa nalo nasikuwa na uwezo wa kununu,” “Mbali na hivyo pia nimpongeze sana Naibu Meya wa jiji la Dar es Salaam, Abdallah Mtinika kwa kujitolea kufufua bima yangu ambayo iliisha na nikashindwa kuifufua, ila GSM

Rais Magufuli ateua Wenyeviti wa Bodi

Image
Rais wa Tanzania, Rais Magufuli ateua Wenyeviti wa Bodi amefanya uteuzi wa wenyeviti watatu  watakaoongoza bodi za taasisi mbili za Serikali na moja ya ubia wa Serikali na Sekta Binafsi.

Dirisha dogo la usajili Ulaya kufungwa leo

Image
Leo ni siku ya hekaheka kwa wahezaji, mawakala na makocha. Ijumaa ya leo Januari 31 ni mwisho wa dirisha dogo la usajili la majira ya baridi. Kufikia saa sita ya usiku kwa saa za Ulaya timu nyingi zinatarajiwa kufanya makubaliano ya mwisho na kuuziana wachezaji. Usajili mkubwa mpaka sasa kwa mwezi huu nchini Uingereza umefanywa na Manchester United jana Alhamisi kwa kumnyakua kiungo Bruno Fernandes kutoka klabu ya Sporting Lisbon. Kocha wa United Ole Gunnar Solskjaer aliahidi kuwa usajili huo ungekamilika kabla ya leo, na wametoa kitita cha pauni milioni 47. Hata hivyo dau hilo linaweza kuongezeka mpaka kufikia pauni milioni 67. Mabingwa hao wa Serie A wamekuwa wakimnyatia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 kwa wiki kadhaa sasa na wanaaminika kuwasilisha ombi la kutaka kumsaini siku ya Alhamisi Robinson alijiunga na Latics kutoka Everton mnamo mwezi Julai 2019 kwa mkataba wa miaka mitatu baada ya kuonyesha mchez

Balozi Kingu naye aitikia wito wa TAKUKURU

Image
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Balozi Mteule, Meja Jenerali Jacob Kingu naye amefika katika ofisi za TAKUKURU jijini Dodoma ili kuhojiwa kufuatia agizo la Rais Dkt. John Magufuli kutokana na mkataba tata wa Tsh trilioni 1.04 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya zima moto. Mwingine aliyewasili leo Ijumaa, Januari 31, 2020, kuhojiwa na TAKUKURU ni aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo, Kangi Lugola ambaye amefika ofisini hapo mapema leo saa 1 asubuhi.

Waziri Kigwangala ampa ubalozi Bongozozo

Image
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Hamisi Kigwangalla, amemtangaza mwanamitandao na mhamasishaji wa timu ya Taifa ya Tanzania, Bongozozo, kuwa balozi wa hiari. Dkt Kigwangalla ametoa taarifa hiyo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, ambapo amepost video fupi ya Bongozozo na kuandika kuwa. "Balozi Bongozozo, umefika wakati sasa nitambue rasmi fujo isiyoumiza kama harakati serious ya kuitangaza Tanzania na Kiswahili chetu, kwanza kwa kumtangaza Bongozozo kama balozi wa hiari wa utalii wa Tanzania" ameandika Hamisi Kigwangalla. "Hivyo naelekeza Bodi ya Utalii Tanzania imuandikie rasmi barua ya kutambua mchango wake na kumtangaza kuwa balozi wa hiari wa utalii, pili kumuandalia safari ya kuja kutalii Tanzania, #TanzaniaUnforgettable" ameongeza. Bongozozo ni Muingereza ambaye amejipatia umaarufu katika mitandao ya kijamii kwa kuongea kiswahili fasaha, anaishabikia timu ya Taifa ya Tanzania pia ameoa mke kutoka Tanzania ila anaishi naye nchini Uingereza.

Waziri Mkuchika afanya uteuzi wa Makatibu tawala wa Wilaya

Image
Waziri Wa Nchi, Ofisi Ya Rais, Menejimenti Ya Utumishi Wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa wilaya nane kwa kuwapandisha vyeo makatibu tarafa na kuwabadirishia vituo vya kazi makatibu tawala watatu.

VIDEO: Mwamuzi aliyechezasha mechi ya Simba na Yanga matatani

Image
Kamati ya saa 72 kupitia kwa Makamu Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi, Ibrahim Mwanyela, ametoa mustakabali wa Bodi ya Ligi na Maamuzi waliofanya kwenye Mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara na Ligi Daraja la kwanza ambapo moja ikiwa mchezo uliowakutanisha Simba SC na Yanga SC na kubaini mapungufu kwenye mchezo huo. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI........USISAHAU KUSUBSCRIBE

VIDEO: Meja Generali Kingu aungana na Lugola, atinga Takukuru kuhojiwa

Image
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ndani ya Nchi, Meja General Jakobo Kingu amewasili Makao Makuu ya TAKUKURU kuhojiwa na mamlaka hiyo. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.......USISAHAU KUSUBSCRIBE

SHULE YA MADANDI SECONDARY SCHOOL INAKUTANGAZIA NAFASI ZA MASOMO

Image
Tunatangaza nafasi za kidato cha kwanza mwaka 2020  na nafasi za kuhamia kwa kidato cha II, III na IV, shule iko katika halmashauri ya mji Kasulu  mkoa wa kigoma. Ada zetu kwa mwaka mzima pamoja na michango ni Tsh. 860,000/= zinalipwa kwa awamu NNE kila awamu 215,000/= tu. Shule inaendeshwa kwa maadili ya kikiristo (Anglikana) na tunaheshimu imani zote pia. Tuna mazingira mazuri ya kujifunzia, maabara pamoja na maktaba iliyosheheni vitabu vya kila namna. Kwa maelezo zaido fika shuleni kwetu au piga Simu 0765 423595 au 0628 738040

Ndugai amvaa Zitto "Umefaidika nini kuandika barua benki ya dunia ili Tanzania ikose mkopo?"

Image
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai, amehoji mwenendo na sababu ya Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe,kuandika barua Benki ya Dunia ili Tanzania ikose fursa ya kupewa mkopo wa elimu kwa sababu ya tofauti za sera Hayo ameyasema leo Januari 31, 2020, katika Mkutano wa 18, Bunge la 11, Kikao cha Nne, wakati wa kipindi cha maswali na majibu juu ya sekta ya elimu na kusema kuwa kitendo alichokifanya Zitto Kabwe si kizuri kwani kinakandamiza haki ya kupata elimu kwa watoto wa wapiga kura wao. "Waheshimiwa Wabunge wakati mwingine mwenendo wetu haueleweki, mwenzetu Zitto Kabwe atakaporudi labda atafafanulia wenzake, kuandika barua World Bank kwamba nchi yetu ikose fursa ya mkopo ambao lengo lake ni elimu, nadhani ni kwenda mbali mno na sijui katika hilo unafaidika nini kwa sababu kama ni tofauti za kisera hayo ni mambo ya kujadili tu, hili limetugusa na kutukera wengi, baadhi yetu hapa watoto wetu wako feza boys, Marian halafu unablock kwa watoto wa wapiga

Kenya Airways yasitisha safari zake kuelekea China kwa hofu ya corona

Image
Shirika la ndege la Kenya limesitisha safari zote za kwenda China baada ya mlipuko wa virusi vya corona. Virusi hivyo vimesababisha vifo 213 nchini China na maambukizi kwenye mataifa mengine 16. Visa sita vya maambukizi vimeripotiwa barani Afrika ingawa wagonjwa waliofanyiwa vipimo wamekutwa kuwa hawana maambukizi ya virusi hivyo. Nchini Kenya, siku ya jumanne, mwanafunzi aliwekwa karantini hospitalini katika mji mkuu Nairobi, baada ya mwanafunzi huyo kutokea katika mji wa Wuhan nchini China, eneo ambalo ndio chimbuko la mlipuko huo. Kenya Airways imesema kuwa bado iko kwenye mazungumzo na wizara ya afya na wizara ya mambo ya nje kuhusu muda ambao ndege hizo zitaacha safari ya China. Lakini safari za mji mkuu wa Thailand, Bangkok, zitakuwa zinaendelea.

THBUB yashauriwa kushirikiana na serikali kuboresha upatikanaji wa haki kwa wananchi

Image
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa taasisi ya Haki za Binadamu Afrika (NANHRI), Gilbert Sebihogo ameishauri Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) kushirikiana na serikali katika kuboresha upatikanaji wa haki kwa wananchi, huku akiwaasa  kujiepusha na vitendo vya kukosoa kila jambo linalofanywa na Serikali. Sebihogo alitoa kauli hiyo Januari 30, 2020 katika ofisi za THBUB zilizopo Dodoma alipozitembelea  kwa lengo la kutambuana na Makamishna wa tume na kuimarisha uhusiano wao wa muda mrefu . Alimueleza Mwenyekiti wa THBUB, Jaji Mstaafu, Mathew Mwaimu kuwa tume itafute namna nzuri ya kuishauri  serikali na kujenga ushawishi utakaofanya serikali iendelee kuwawezesha kutekeleza majukumu yao. “Tume mnapaswa kuendelea kuishawishi serikali kufanya nao kazi kama washirika, mfanye kazi bila misuguano wala kudharau mambo mazuri yanayofanywa na serikali, kwa kufanya hivyo kutaifanya serikali kushirikiana na nyinyi”, Sebihogo alisisitiza “Msiwe wakosoaji wa  kila jambo kama baad

Msemaji wa serikali: Uchumi wa Tanzania umekua kwa 6.9%

Image
Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi amesema kwa takwimu za mpaka September 2019, uchumi wa Tanzania umekua kwa 6.9% huku matarajio yakiwa ni kufikia hadi 7.1% “kwa Afrika Mashariki tunahangaika na Rwanda, kwa Nchi za SADC Tanzania ni miongoni mwa Nchi ambazo zinaongoza kwa uchumi wake kukua kwa kasi" . "Uchumi unaokua unaweza kuupima kwa namna nyingi mojawapo ni maisha ya Watu, Tanzania ukienda Shule elimu bure, angani kazi zinafanyika, vyuo vikuu ada Wau wanalipiwa, kuakisi kwa uchumi kukua maana yake ni uwezo wa Serikali kufanya mambo mengi" - Dr. Abbas . "Katika Ripoti ya Transparency 2019 ya January 23, 2020, Tanzania imekuwa ya 96 kutoka ya 117 mwaka 2015 na 103 mwaka 2017, kwa matokeo haya Tanzania ni ya pili kwa Afrika Mashariki kwa kutokuwa na rushwa nyuma ya Rwanda"- Dr. Abbas.

Simba, Yanga kuonyeshana ubabe machi 8

Image
MECHI ya marudiano ya watani wa jadi ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2019/20, Yanga dhidi ya Simba imepangwa kufanyika Machi 8, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa ratiba hiyo iliyotolewa na Bodi ya Ligi kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), jana mwenyeji wa mchezo huo ambao wa raundi ya 28 ni Yanga inayofundishwa na Kocha Mkuu Mbelgiji Luc Eymael. Katika mechi hiyo, timu hizo zitashuka dimbani zikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare ya mabao 2-2, ambayo walipata katika mchezo wa mzunguko wa kwanza iliyochezwa Januari 4, mwaka huu jijini. Matokeo hayo bado yamekuwa yakiwaumiza mashabiki wa Simba baada ya kuamini timu yao ingeondoka na pointi tatu na yakionekana kufurahiwa na Yanga ambayo ilidhani 'jahazi' lao limezama baada ya kuwa nyuma kwa magoli 2-0. Magoli ya Simba inayonolewa na Sven Vandenbroeck, raia wa Ubelgiji katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Jonesia Rukyaa kutoka Bukoba yalifungwa na Meddie Kagera na De

VIDEO: Breaking News, Lugola atinga TAKUKURU kuhojiwa, abeba ilani ya CCM

Image
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya ndani Kangi Lugola leo majira ya saa moja na nusu kwa kwa saa za Afrika Mashariki amewasili katika ofisi za Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU, Jijini Dodoma kwa ajiri ya kuhojiwa na Mamlaka hiyo. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI......USISAHAU KUSUBSCRIBE

NIDA yasitisha kutoa copy za vitambulisho mtandaoni

Image
Mamlaka ya Vitambulisho Taifa NIDA imesitisha huduma na matumizi ya nakala tepe ya kitambulisho cha Taifa ya mitandaoni online ID copy

Serikali yachukua tahadhari kuhusu tishio la Nzige

Image
Kutokana na taarifa za kuwepo kwa tishio la kuvamiwa na nzige wa jangwani hapa nchini serikali imeanza kuchukua tahadhari ya kuratibu upatikanaji wa viuatilifu maalum Zaidi ya lita 7,000 vya kuwadhibiti nzige hao. Mapema mwishoni mwa mwaka jana 2019 nzige wa jangwani waliripotiwa kushambulia maeneo ya kaskazini mwa nchi jirani ya Kenya wakitokea Eritrea na Ethiopia na kuchukua uelekeo wa kusini takribani kilomita 166 kutoka ulipo mpaka wa nchi hiyo na Uganda. Serikali ya Tanzania imeanza kuchukua tahadhari ya kuwadhibiti nzige hao endapo wataingia hapa nchini pamoja na visumbufu wengine wakiwamo ndege aina ya kwelea kwelea, viwavi jeshi na nzige wekundu. Waziri wa kilimo Japhet Hasunga amebainisha kuwa nzige hao wana madhara makubwa kwa mazao ya chakula, mimea na uoto wa asili. Tahadhari inatolewa kwa wananchi hususani wakulima kutoa taarifa kwa uongozi wa serikali za vijiji endapo watabaini uwepo wa wadudu wasiowafahamu ili wizara itume timu ya wataalam kuwachunguza. Hii s

Picha: Lugola kuhojiwa leo, hivi ndivyo alivyotinga TAKUKURU

Image
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amewasili Makao Makuu ya Ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) jijini Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa. Lugola anadaiwa kusaini ununuzi wa vifaa vya zimamoto na uokoaji vyenye thamani ya Tsh trilioni 1.04 kutoka kampuni ya nje ya nchi bila kufuata sheria.

Burundi : Wanahabari 4 wahukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 2 jela

Image
Mahakama moja magharibi mwa Burundi Alhamisi imewahukumu kifungo cha miaka 2 na miezi 6 wanahabari 4 wa gazeti la Iwacu, kwa shutma za kufanya jaribio la kuvuruga usalama wa taifa, gazeti hilo limeripoti kwenye mtandao wake wa twitter. Iwacu imeongeza kuwa dereva wake aliyekuwa anashutumiwa pamoja na wanahabari hao yeye amekutwa hana hatia na ameachiwa huru. Mahakama imeomba pia wanahabari hao kulipa faini ya faranga milioni 1 za Burundi, sawa na dola za Marekani 529. Mkurungezi wa gazeti hilo, Antoine Kaburahe ameitaja hukumu hiyo kama aibu kwa vyombo vya sheria nchini humo. “Sisi tunafikiri majaji wamepewa shinikizo la kutowaachia huru wanahabari wetu. Ukitizama uzito wa kosa wanalotuhumiwa la kutaka kuvuruga usalama wa taifa, haileweki kuona wamepewa hukumu ndogo kama hiyo,” Kaburahe ameiambia Sauti ya Amerika. “Majaji wameshindwa kutekeleza wajibu wao wa kutenda haki," ameongeza. Kaburahe amesema watakata rufaa. Wanahabari Christine Kamikazi, Agnes Ndirubusa, Teren

Shirika la afya duniani latangaza corona kuwa janga la dunia

Image
Virusi vipya vya corona vimetangazwa kuwa janga la dharura,wakati virusi hivyo vikiendelea kusambaa kwa kasi nje ya China, kwa mujibu wa shirika la afya duniani(WHO). "Sababu kubwa ya tangazo hilo si kwa sababu ya kile ambacho kinatokea China kwa sasa lakini kile ambacho kinatokea katika mataifa mengine," alisema kiongozi mkuu wa shirika la afya duniani Tedros Adhanom Ghebreyesus . Kinachoangaziwa zaidi ni kuhusu ugonjwa huo kusambaa mataifa mengine huku kukiwa na mfumo duni wa afya Shirika la afya duniani limesema kuwa kumekuwa na visa 98 katika mataifa mengine 18 ingawa hakuna vifo vilivyobainika. Visa vingi vya wagonjwa hao walikuwa wamesafiri kutoka mji wa Wuhan, eneo ambalo mlipuko wa ugonjwa huo ulianza. Hata hivyo kuna kesi nane zilizosababishwa na maambukizi ya kati ya mtu kwa mtu huko Ujerumani, Japan, Vietnam na Marekani. Akizungumza katika mkutano wa habari Geneva, Dkt Tedros alielezea virusi vya corona kuwa mlipuko wa ugonjwa ambao haujawahi kutokea aw

Wataalamu wa kilimo cha umwagiliaji wajadiliana juu ya kuwajengea uwezo wakulima

Image
Wataalam wa kilimo cha umwagiliaji wameendelea na majadiliano Jijini Dodoma huku, wakibadilishana mawazo na uzoefu kuhusiana na Mradi wa kuwajengea uwezo wakulima na wataalam katika Kilimo cha Umwagiliaji wakijikita zaidi katika shughuli za mradi huo,mafanikio na Changamoto na namna ya kutatua changamoto hizo ambazo zinaweza kupelekea Mradi huo kuwa endelevu hata baada ya muda wake kufikia mwisho. Wataalam hao walifanya mawasilisho ya Mpango kazi kupitilia utekelezaji wa mradi, kama vile kazi za upembuzi yakinifu katika miradi ya kilimo cha umwagiliaji ambayo hufanyika kabla ya mradi kuanza na mradi kutekelezeka, jambo ambalo linapelekea ubora na uimara wa miundombinu ya umwagiliaji. Sambamba na hilo, mawasilisho pia yalilenga katika majadiliano yaliyohusu tathmini na ufuatiliaji katika swala zima la matumizi na matunzo ya miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji hasa katika eneo la matunzo ya miundmbinu hiyo. Mradi huo ulianza kazi kwa awamu ya kwanza kutoka December 2010 mpaka J