Posts

Showing posts from September, 2019

Rais Magufuli afanya teuzi mbalimbali

Image
Rais John Magufuli amefanya teuzi mbalimbali za Wakurugenzi wa Halmashauri za Manispaa na Wilaya, Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocal) na Uhamisho wa Wakurugenzi wa Halmashauri.

Madiwani Tanzania waagizwa kutoa Majina ya Mitaa

Image
Serikali imewataka madiwani wote nchi nzima kutoa majina ya mitaa ili kufanikisha utekelezaji wa mpango wa anwani za makazi na postikodi. Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye wakati akifungua mafunzo ya kujenga uelewa kuhusu umuhimu na manufaa ya kutekeleza mpango wa anwani za makazi na postikodi kwa madiwani, viongozi wa Serikali na watendaji mbali mbali wa Mkoa wa Kigoma yaliyofanyika wilayani Kibondo yaliyotolewa na wataalamu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa pamoja na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania “Madiwani tupeni majina ya mitaa ili vifurushi, barua na vipeto viwe vinakwenda moja kwa moja kwa wananchi, tufanye biashara mtandao na kuimarisha ulinzi na usalama,” amesema Nditiye Ameongeza kuwa biashara mtandao ni nzuri, tunataka kifurushi cha mtu kiletwe anapoishi na tayari nchi nzima kata zote zina postikodi, madiwani tupeni majina ya mitaa ili tuweke vibao na namba za nyumba ili wananchi watambulike “Unawe

Rais Magufuli amteua Mkurugenzi mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)

Image
Rais Magufuli amemteua Dkt. Wilson Mahera kuwa Mkurugenzi mpya wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) akichukua nafasi ya Athuman Kihamia ambaye atapangiwa kazi nyingine. Kabla ya uteuzi huo Mahera alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Arusha

Walimu wametakiwa kujiendeleza kielimu

Image
Na Thabit Madai, Zanzibar Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi, Hassan Khatib Hassan amewataka walimu wa Shule za msingi katika Mkoa huo kujiendeleza kielimu ili kuongeza mbinu mbali mbali za ufunishaji nakuongeza ufaulu wanafunzi. Wito huo ameutoa wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya  walimu wa shule  za msingi ndani ya Mkoa Mjini Magharibi uliofanyika katika ukumbi wa kituo cha walimu Bububu Mjini Unguja. Mafunzo hayo kwa walimu yameandaliwa na Taasisi ya Rafiki Elimu. Mkuu huyo wa Mkoa alisema suala la kujiendeleza kielimu kwa walimu litaongeza kasi ya mabadiliko na ukuwaji wa sekta ya elimu nchini hatua ambayo itaongeza wataalamu wa fani mbalimbali na kuwa na taifa lenye wasomi. "Kazi hiyo ya ualimu ni kazi ambayo inahitaji mabadiliko hususan katika suala la kuongeza uwezo wa kitaalamu kujiendeleza ni jambo la msingi ili muweze kuwaanda vijana wetu wapende elimu na skuli na wapunguze mda wa kubaki nyumbani". Aidha Hassan alisema  Serikali ya Mkoa huo itaendelea kusimam

Kigogo CUF atimkia CCM

Image
Mwanachama Mkongwe wa Chama cha Wananchi (CUF) aliyekuwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Singo Kata ya Gongoni katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Hamisi Mwami (53) amekihama chama hicho na kujiunga CCM. Mwami ambaye amekuwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo kwa miaka 20 sasa amesema kuwa ameamua kuhamia CCM kwa utashi wake mwenyewe baada ya kusoma alama za nyakati na kuridhika na utendaji wa Rais John Magufuli. “Nimesoma alama za nyakati, upinzani hauna la kusema sasa hivi ndio maana nimeamua kuhamia CCM kwa utashi wangu na sio kwa kununuliwa au kushawishiwa na mtu kwani nina uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika siasa sasa nimekuwa kiongozi wa Serikali hivyo nina upeo wa kuona mbali”, amesema. Aidha amesema uroho wa madaraka unaokitafuna chama cha CUF na vyama vingine vya upinzani ni miongoni mwa mambo ambayo yamedhoofisha upinzani hapa nchini na hivyo kushindwa kuwa watetezi wa wananchi,  ndiyo maana ameamua kujiunga na timu ya watu makini wanaojali sana maslahi ya wan

Makamu wa Rais akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Denmark, Ufaranza na Qatar hapa nchini

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Denmark hapa Nchini Bibi. Mette Norgaard Dissing Spandet wakati Balozi Spandet alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikuklu Jijini Dar Es salaam Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Ufaransa hapa Nchini Bw. Frederic Clavier wakati Balozi Clavier alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikuklu Jijini Dar Es salaam  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Balozi wa Qatar hapa Nchini Bw. Abdulla Jassim Al-Maadadi wakati Balozi Al-Maadadi alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikuklu Jijini Dar Es salaam

MAGAZETI YA LEO 1/10/2019

Image

Huu msamaha sio wa uongo narudia tena - Rais Magufuli

Image
Rais Magufuli ameongeza siku saba zaidi kwa watuhumiwa wa rushwa na uhujumu uchumi kuomba msamaha baada ya DPP kuomba aongezewe siku tatu kutokana na wengine kushindwa kukamilisha taratibu za kisheria kwa wakati. Rais Magufuli amesema hakutegemea kama watuhumiwa 467 wa kesi za uhujumu chumi wangeandika barua wakiomba wasamehewe, huku akimueleza DPP kuwa anafahamu kuna barua nyingine zimekwama kwenye ofisi zako za Mikoa, na kama kweli wapo waliokwamishwa kwa sababu ya umbali, "Natoa wito kwa Watanzania wenye tuhuma za uhujumu uchumi, wasiwe na wasiwasi kwamba ukishakiri basi kesho ndiyo ushahidi huo, siwezi nikafanya kazi ya kitoto namna hiyo, nimeshasema nimetoa msamaha ni msamaha kweli,hakuna msamaha wa majarbio au wa kumtega mtu, wasidanganywe" amesema. "Katika siku 7 wapo ambao walizuiliwa na Maofisa wa Magereza wakitaka hongo kidogo kwamba unatuachaje hapa ndani,Kamishina wa Magereza upo hapa mkafuatilie waliomba msamaha kwa DPP msiwakwamishe, hizi Bilioni 10

Wawekezaji watakiwa kuyaongezea thamani Maziwa kufika soko la Nje

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amekutana na wawekezaji kutoka Jamhuri ya Ireland wenye nia ya kuwekeza katika sekta ya maziwa hapa nchini na kuwataka kuangalia zaidi mnyororo wa thamani wa namna ya kuyaongezea thamani maziwa ili kupanua zaidi soko la maziwa kutoka Tanzania kwenda nchi za nje. Akizungumza na wawekezaji hao leo kutoka shirika la Sustainable Food Systems Ireland (SFSI) ofisini kwake katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, Prof. Gabriel amesema maziwa yatakapoongezewa thamani yataiwezesha Tanzania kuingia zaidi katika masoko ya nje ya nchi yakiwemo ya Afrika Mashariki na Jumuiya ya Ushirikiano na Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) “Waangalie pia zaidi mnyororo wa thamani namna ya kuyaongezea maziwa thamani ili tuingie zaidi katika solo la Afrika Mashariki, SADC na nje ya SADC. Lengo kubwa la wizara kwa wadau kama hawa wakija kutuona inakuwa faraja kwa kuwa inagusa maisha ya mfugaji wa kawaida, pale amba

Wanawake watakiwa kujitokeza kuwania nafasi za uongozi 2020

Image
Na Thabit Madai, Zanzibar Wanawake Nchini wametakiwa kuchangamkia fursa ya kuwania nafasi mbali mbali za uongozi katika Uchaguzi Mkuu ifikapo mwakani 2020.  Wito huo umetolewa na Ali Haji Ubwa mwenyekiti wa kamati ya kushajihisha wanawake kushika nafasi mbalimbali za uongozi katika wilaya ya kaskazini A Unguja.  Ali Haji Ubwa alisema kuwa baadhi ya wanawake katika jamii hususani ya Zanzibar wamekuwa na muamko mdogo katika kugombania nafasi mbali mbali za uongozi nakubakia kuwa nyuma  katika masuala yamaendeleo. Alisema wanawake kutokuwa katika nafasi mbali mbali za uongozi hupelekea kurudishwa nyuma kimaendeleo  na kuwa tegemezi katika jamii kutokana kuwa baadhi ya mambo yao kila siku yataendelea kuamuliwa na baadhi ya viongozi kwa maslahi yao.  “Ukweli kwamba wakina mama (wanawake) wanakabiliwa na changamoto nyingi sana lakini  hakuna wa kuwasemea katika ngazi za maamuzi hivyo mimi kama mwenyekiti nawashauri kuwa wajitokeze katika kuwania nafasi mbali mbali za uongozi kwa

RC Mtwara ataka vijana kujiandaa na maisha ya uzeeni

Image
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Bw. Gelasius Byakanwa amewataka vijana ambao bado wana nguvu za kufanya kazi kujiandaa vyema na maisha ya uzeeni ili kuepuka kutoa lawama na kulalamikia Serikali katika maisha yao ya uzeeni. Aidha Kiongozi huyo nameiomba Serikali iangalie uwezekano wa kutunga Sheria ambayo itaainisha majukumu ya watoto kwa wazee, majukumu ya wazee kwa watoto pamoja na majukumu ya Serikali kwa wazee ikiwemo haki ya kulinda wazee kama ilivyo sheria ya Mtoto ya mwaka 2009. Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bw. Byakanwa  amesema hayo leo wakati wa akizindua Maadhimisho ya Kimataifa ya Siku ya Wazee Duniani yanayoadhimishwa Kitaifa Mkoani Mtwara  kwa Siku tatu kuanzia Septemba 29, na kufikia kilele chake Octoba 1, 2019. Mkuu wa Mkoa wa Mtwara aliongeza kuwa wakati wa utunzi wa sheria ya wazee majukumu mengi yasirundikwe kwa Serikali lakini sheria hiyo iyaangazie majukumu hayo kwa jamii ili ione umuhimu wa kuwa na wajibu wa kuwatunza wazee. Bw. Byakanwa pia ametoa angalizo kwa viongozi

VIDEO: Wahujumu uchumi 467 watubu kwa Rais Magufuli

Image
Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP), Biswalo Mganga amesema ofisi yake imepokea barua za watuhumiwa 467 wanaoomba kukiri makosa ya uhujumu uchumi na wapo tayari kurudisha fedha jumla ya Sh107.8 bilioni. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI...USIKOSE KU SUBSCRIBE

SHULE YA MSINGI CHIPOLE INAWATANGAZIA NAFASI ZA MASOMO

Image
UONGOZI WA SHULE YA MSINGI YA SHIRIKA LA MTAKATIFU AGNES  CHIPOLE. UNAPENDA KUWATANGAZIA NAFASI ZA MASOMO KWA WAVULANA NA WASICHANA MWAKA 2020. SHULE IPO KATIKA MKOA WA RUVUMA WILAYA YA SONGEA INAPOKEA WANAFUNZI KUANZIA DARASA LA I, II, III, IV, V NA VI. TAREHE YA KURIPOTI  KWAAJILI YA USAHILI NI  OKTOBA, 11, 2019  HUKU TAREHE YA MTIHANI IKIWA NI  12 OKTOBA 2019  SAA 2:00 ASUBUHI. ADA YA MTIHANI NI TSH. 10,000/- SHULE  NI YA BWENI YENYE MCHANGANYIKO WA WAVULANA NA WASICHANA NA YENYE WALIMU MAHIRI NA WAZOEFU KATIKA UFUNDISHAJI. “SHULE INAPOKEA WANAFUNZI WA MADHEHEBU YOTE”. TANGAZO HILI LINAPATIKANA KATIKA VITUO VIFUATAVYO: SHULE YA MSINGI CHIPOLE NO. 0756-961896 /  0717-439469 DAR – ES – SALAAM, ST. SCHOLASTICA PRIMARY SCHOOL  ( MZAMBALAUNI ) NO. 0656728332. KYELA DUKA LA NGAYOCHA KYELA SOKONI KARIBU NA DUKA LA DAWA LA MZOMOZI NO. 0762787831/ 0682624862 / 0714088486 NDANDA – MADEKO NO. 0718412358 SONGEA – ST. ANDREW (BOOK BINDING) JIMBONI MBINGA -  ST