Posts

Showing posts from May, 2019

TANGAZO: TATIZO LA KUTOKUONEKANA KWA PICHA LIMEKWISHA RASMI

Image
Tunaomba radhi kwa tatizo la kuto kuonekana kwa picha kwa Baadhi ya watumiaji wetu wa App ya Muungwana Blog. Tunapenda kuwataarifu kuwa tatizo hilo limekwisha Rasmi, kama bado unatatizo hilo basi ingia  PLAY STORE  kisha andika MUUNGWANA BLOG kisha  UPDATE  App yetu. Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza katika kipindi hiki chote. Kwa Maoni au maswali wasiliana nasisi kupitia namba hizi  0719788949 - 0789547574

MAGAZETI YA LEO 1/6/2019

Image

Rais Ramaphosa wa Afrika Kusini achagua Baraza la Mawaziri

Image
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amechagua Baraza jipya la Mawaziri, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kupambana na rushwa iliyotawala katika serikali yake. Ramaphosa ameonya kwamba mawaziri hao watafuatiliwa kwa karibu, Baraza hilo jipya lina mawaziri 28 badala ya 36 wa baraza lilopita na nusu yake ni wanawake. Ramaphosa amechagua mawaziri wake kutoka ndani na nje ya chama chake cha African National Congress (ANC).  Matarajio ni makubwa miongoni mwa wanachi wa Afrika Kusini, waliokichagua tena chama cha ANC katika uchaguzi wa Mei 8. Wanamtegemea Ramaphosa kuleta mfumo mpya wa uongozi baada ya taifa hilo kwa miaka kadhaa kukabiliwa na kashfa tofauti.  Kuteuliwa tena kwa David Mabuza kama Naibu Rais kumezua malalamiko kutoka upande wa upinzani. Jina la Mabuza limehusishwa na rushwa na tume ya uadilifu ya chama cha ANC.

Waislam watakiwa kushirikiana kiimani katika shughuli za maendeleo

Image
Na Rahel Nyabali,Tabora Waislam mkoani Tabora wametakiwa kuondoa tofauti zao kwa kushirikiana katika kumcha Mwenyezi Mungu  kuwa wa moja kiimani na katika shughuli za kimaendeleo ya kijamii ili kuimarisha umoja miongoni mwao bila kubaguana katika misikiti ya ibada. Wito huo umetolewa na Sheikh wa Mkoa wa Tabora Alhaj Ibrahim Mavumbi  wakati akiongea na Masheikh wa wilaya wa mkoa wa Tabora ofisini kwake amewataka masheikh kuandaa vijana wakiislamu kwa ajili ya mashindano ya kuhifadhi judhuu ambayo yatahudhuriwa na waumini wa dini mbalimbali juni 13 mwaka huu mjini Tabora. Katika kikao hicho Sheikh Mavumbi amewaomba waumini wa dini ya kiislam kuendelea na funga yao ya mwezi mtukufu wa ramadhani kwa kufuata misingi yote ya dini bila kusahau kumcha Mwenyezi Mungu. Aidha Wakiongea kwa niaba ya Masheikh wenzao Sheikh wa wilaya ya Nzega Mrisho Zahor na  Zaimu Ramadhan  kaimu Sheikh wa Urambo  wameahidi kusimamia maelekezo hayo kwa kuwaelimisha waumini wao, na kuhakikisha  umoja na

Sijawahi kujaribu kuomba msamaha WCB - Rich Mavoko

Image
Msanii wa Bongo Fleva, Rich Mavoko amesema alishtushwa na taarifa zilizokuwa zinasambaa mtandaoni kuwa ameomba msamaha ili arudi kufanya kazi na lebo ya WCB. Akizungumzia ishu hiyo, Mavoko ambaye alijitoka WCB mwaka jana, alisema alisikia taarifa hizo za kizushi kupitia mdogo wake lakini baada ya kufuatilia aligundua ni uongo hivyo akapuuzia. "Sijawahi kujaribu kuomba msamaha na hakiwezi kutokea kitu kama hicho, bora nivae shati lililochanika kuliko kutembea tumbo wazi, kikubwa naomba mashabiki zangu waendelee kunipa sapoti kupitia wimbo wangu mpya Usizuge,” Mavoko ameimbia Clouds FM. Kwa sasa Rich Mavoko anafanya vizuri na wimbo wake unaokwenda kwa jina la Usizuge kutoka chini la lebo ya Bilionea Kid.

Waamuzi atakaocheza fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC)

Image
Nahodha wa Lipuli FC Ally Mtoni (Kulia) na Agrey Moris wa Azam FC (Kushoto) wakitakiana mchezo wa Kiungwana kuelekea Fainali ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) itakayochezwa Kesho Jumamosi Juni 1,2019 Uwanja wa Ilulu,Lindi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limemtangaza Hance Mabena (pichani) kutoka Tanga kuwa mwamuzi wa mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC) utakaopigwa kesho Juni 01, 2019. . Katika mchezo huo watatumika waamuzi sita kwa mara ya kwanza kwenye historia ya soka la Tanzania ambapo Mabena atasaidiwa na jumla ya waamuzi watano (wawili wa pembeni , wawili wa kwenye magoli na mwamuzi mmoja wa akiba). . Mfumo wa kuwa na waamuzi sita ulianza kutumiwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwenye AFCON ya vijana chini ya miaka 17 iliyofanyika nchini mwezi Aprili 2019. Kwa mujibu wa taarifa ya TFF iliyotolewa leo, Hance Mabena atasaidiwa na Mohamed Mkono kutoka Tanga kama mwamuzi msaidizi namba moja, Frednarnd Chacha kutoka Mwanza kama mwam

Mama mjamzito ajifanyia operesheni kwa kutumia wembe

Image
Mbunge wa Nkasi Kaskazini Ally Kessy amelalamikia juu ya uwepo elimu hafifu hususani kwa baadhi ya kinamama, na kueleza imepelekea mama mmoja ambaye alikuwa ni mjamzito jimboni kwake kujifanyia operesheni mwenyewe, kwa kutumia wembe bila kwenda Hospitali. Akizungumzia katika kipindi cha maswali na majibu Bungeni jijini Dodoma, Mbunge Kessy ameeleza mama huyo kwa sasa hali yake ni mbaya zaidi, lakini alifanikiwa kujifungua na mtoto wake anaendelea vizuri. Mbunge Kessy amesema kuwa "vifo vingine vya kinamama vinatokana na kina mama wenyewe,  juzi tu jimboni kwangu kuna mama mmoja tena zao lake la nane, kachelewa mwenyewe makusudi kwenda kituo cha afya" "Yule mama akaamua kujifanyia oparesheni mwenyewe kwa kutumia wembe na katoa mtoto, sasa hivi yuko Hospitali hali yake si nzuri ila hali ya mtoto ni nzuri, kwa hiyo wakati mwingine vifo vya kina mama vinatokana na wao wenyewe" amesema Mbunge Kessy.

Watumishi wapya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wapigwa msasa

Image
Ofisi ya Wakili Mkuuwa Serikali kwa kushirikiana na Chuo cha Utumishi wa Umma imeendesha mafunzo elekezi kwa watumishi wapya kwa lengo la kuwajengea uwezo na kuhakikisha inatoa huduma bora na yenye viwango. Mafunzo hayo yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, yamewahusisha watumishi wapya ambao ni Mawakili, Afisa Kumbukumbu, Afisa Tehama pamoja na Afisa Habari. Akizungumzia mafunzo hayo Mkurugenzi wa Utawala na Rasirimali Watu Bw. James Kibamba, amesema mafunzo hayo ni muhimu kwani yamelenga kuwajengea uwezo wa kimaadili watumishi wapya ili waweze kufanya kazi zao kwa mujibu wa Sheria na taratibu za Utumishi wa Umma. “Mafunzo haya ni muhimu sana hasa kwa Watumishi wapya katika utumishi wa Umma kwa kuwa yanawasaidia kujua taratibu zote za kiutumishi ndani ya Utumishi wa Umma”. Alisema Bw. Kibamba. Aidha Bw. Kibamba amewaasa watumishi hao kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuzingatia masuala ya kinidhamu katika nyanja zote sambasamba na kuwaheshimu watumishi weng

R. Kelly aongezewa mashitaka mengine 11

Image
R.Kelly ameshtakiwa kwa makosa 11 ya unyanyasaji wa kingono, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya nchini Marekani. Mahakama imeripotiwa kuonyesha kuwa vitendo hivyo vilifanywa dhidi ya watoto wa umri kati ya miaka 13 na 16, na ikiwa itathibitika atakabiliwa na adhabu kali kuliko adhabu nyingine anazokabiliwa nazo. Mwanzoni mwa mwaka huu msanii huyo wa miondoko ya R&B alikabiliwa na mashtaka 10 ya unyanyasaji wa kingono. Alikana kuhusuka na vitendo hivyo na akaachiwa huru kwa dhamana. Ikiwa atakutwa na hatia kwa mashtaka ya awali, yaliyohusisha wanaodaiwa kuwa waathirika wa vitendo hivyo, wakiwemo wasichana wadogo watatu,atakabiliwa na kifungo cha miaka mitatu mpaka saba gerezani. Wakili wa R.Kelly Steve Greenberg amesema mashtaka ya sasa si kwamba ni kesi mpya. ''Ameshtakiwa kwenye kesi ambayo bado ipo, ikihusisha watu walewale wanaodaiwa kuwa waathirika na muda uleule (miaka 10 iliyopita) hakijabadilika kitu'', aliandika kwenye ukurasa wa Twitter. '

Bingwa wa ngumi uzito wa juu duniani Antony Joshua kuzichapa na Andy Ruiz

Image
Bingwa wa ngumi uzito wa juu duniani,Antony Joshua amefanya mazoezi ya wazi mjini New York kuelekea pambano lake hapo kesho Juni 1 na Andy Ruiz mjini humo siku ambayo pia mabondia wa kike Delfine Persoon na Katie Taylor watapigana. Joshua mwenye urefu wa futi sita kwa sasa anashikilia mataji matatu kati ya manne; IBF, WBA na WBO akiwa na rekodi ya kushinda mapambano yake yote 22, kati ya 21 kwa knockout. Ruiz mwenye urefu wa futi nne amepoteza pambano moja na kushinda 32, huku 21 akishinda kwa knockout pia.

Kauli ya Meddie Kagere baada ya kushinda tuzo mbili

Image
Mshambuliaji wa Simba SC, Meddie Kagere amefunguka mara baada ya usiku wa jana kushinda tuzo mbili za MO Simba Awards 2019. Tuzo hizo ambazo zilitolewa jana katika hoteli ya Hyatt Regency - The Kilimanjaro iliyopo Jijini Dar es Salaam, Kagere ndiye mchezaji pekee aliyeshinda tuzo mbili. "Ushindi huu haujaja kwa mimi binafsi, umekuja sababu ya wachezaji wenzangu tunaelekezana jambo ambalo limenisaidia kushinda, najivunia uwepo wao” amesema. Tuzo alizoshinda Kagere ni Mchezaji Bora wa Mwaka na Mfungaji Bora wa Mwaka.

Nyumba 2,000 za bei nafuu kujengwa Kigali Rwanda

Image
Uzinduzi wa nyumba 2,000 za makaazi zenye bei nafuu unatarajiwa kufanyika kesho karika eneo la Nyamirambo mjini Kigali Rwanda. Mradi huo ni ubia kati ya shirika la hazina ya kujenga nyumba la Shelter Afrique, na benki ya maendeleo ya Rwanda. Eneo hilo litakalojulikana kama Rugarama Park Estate litakuwa pia na nyumba soko, maduka na bustani. Takwimu za shirika la Planet Consortium zinaonyesha kuwa mahitaji ya kila mwaka ya nyumba maeneo ya mijini ni nyumba 31, 279 lakini zinazojengwa ni 1,000 tu.

MO Dewji azungumzia usajili wa Ibrahim Ajibu kwenda Simba SC

Image
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Simba SC, Mohamed Dewji ametoa neno kuhusu mipango ya usajili ndani ya timu hiyo na kusisitiza kuwa bajeti ya usajili msimu huu itakuwa mara mbili ya ile ya msimu uliopita. Mo Dewji amezungumza hayo muda mfupi kabla ya kutolewa kwa Tuzo za Mo (MO Simba Awards 2019) zilizofanyika jana kwenye Hotel ya Hyatt Jijini Dar es Salaam. Amesema mipango waliyonayo kwanza ni kuhakikisha wachezaji wote wazuri wanaendelea kubaki ndani ya Simba na kisha kusajili wachezaji wengine wapya wenye uwezo. "Wana Simba wasiwe na wasiwasi hao wachezaji wa ndani tutawabakisha kwa gharama yoyote, lakini pia tutaendelea kutafauta wachezaji wazuri na bajeti ipo," amesema. Pia amesisitiza kuwa hadi sasa bado hawajaanza mchakato wowote wa usajili likiwemo suala la Nahodha wa Yanga SC Ibrahim Ajibu ambaye anahusishwa kujiunga na timu hiyo. MO ameendelea kwa kusema, "Suala la Ibrahi Ajibu kwa ukweli hili jambo hatujakaa na kulimaliza, kwa hiyo kwenye waka

TANZIA: Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Yanga afariki Dunia

Image
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Yanga Advocate Felix Kibodya amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Katika Hospital ya Lugalo baada ya kuugua kwa Muda mfupi. Yanga SC itakumbuka na kuuenzi mchango wake mkubwa kwa timu. Mungu ampumzishe mahali pema peponi.

Wanawake walioolewa hufanyiwa ukatili zaidi

Image
Wizara ya afya maendeleo ya jamii  jinsia wazee na watoto imesema kuwa asilimia 40 ya wanawake nchini wenye miaka 15 hadi 19 wameripotiwa kufanyiwa ukatili wa kimwili huku asilimia 17 ya wanawake wenye miaka 15 hadi 49 wakifanyiwa ukatili wa kingono. Akizungumza Mkurugenzi msaidizi wa masuala ya Watoto Bwana Sebastian Kitiku amesema takwimu hizo ni wale ambao wameripoti lakini wengine wananyamaza kimya bila kutoa taraifa wanapofanyiwa ukatili. Bwana Kitiku amesema kuwa nusu ya wanawake waliokwisha kuolewa asilimia 85 wamefanyiwa ukatili wa kimwili na asilimia 39 ukatili wa kiakili ambapo wanaofanya hayo ni wenza wao wa karibu na kiwango hicho ni kikubwa. ””Kina mama wanafanyiwa sana ukatili na ukatili wa kimwili unaoongoza sana,vipigo kwa kila wanawake 100 waliolewa 39 wanapigwa ,wanajeruhiwa miili na wengine kuathirika kisaikolojia ni wangapi sasa wanafanyiwa ukatili huo na wanamua kuficha siri za wanaume zao” Amesema Kitiku Hata hivyo ameongeza kuwa asilimia 54 ya wanawake

DC akanusha mtu kujinyonga bali alinyongwa

Image
Na James Timber, Mwanza Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Emmanuel Kipole amethibitisha Mkazi wa kijiji cha Nyakahako Kata Chifunfu Wilaya Sengerema mkoani Mwanza Tumaini Faustine (35) aliyeripotiwa kuwa amejinyonga  alinyongwa na watu wasiojulikana kisha mwili wake kutelekezwa juu ya mti. Kipole alisema kuwa kifo cha kijana huyo kinazua utata kwa kuwa alikutwa na majeraha shingoni huku Kichwani akiwa amepigwa na kitu chenye nchi kali pamoja na damu kutoka masikioni suala lililozua utata mkubwa Kipole alieleza kuwa siyo kawaida kwa mtu aliyejinyonga kumkuta anajeraha shingoni kichwani huku akivuja damu masikioni dalili hizo zinadhihilisha wazi kuwa alinyongwa kisha mwili wake kutundikwa juu ya mti. "Jeshi la polisi bado linafanya uchunguzi juu tukio hilo ili kuwabaini watu walihusika kwenye tukio hilo na hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale watakaobainika," alisema Kipole. Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu Kituo cha Afya ya Ngomamtimba kilichoko Kata ya Chifunfu Joh

Ufilipino yarudisha shehena ya takataka Canada

Image
Ufilipino imerejesha tani za takataka nchini Canada, baada ya mvutano wa kidiplomasia wa majuma kadhaa ambapo Rais wa nchi hiyo Rodrigo Duterte kutishia '' kusafirisha takataka kwa njia ya maji kuelekea Canada''. Ufilipino imesema takataka hizo ziliwekwa nembo kimakosa kuwa zilikua za plastiki tayari kwa kutengenezwa upya (recycling) zilipofikishwa Manila mwaka 2014.. Makontena 69 ya takataka yalirejeshwa yakiwa kwenye meli ya mizigo kutokea ghuba ya Subic, kaskazini mwa mji wa Manila. ''Baaaaaaaaa bye, tusemavyo,'' Waziri wa mambo ya nje wa Ufilipino Teddy Locsin Jr aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter Ijumaa asubuhi. Waziri, ambaye amekua maarufu kwa mtindo wa kauli zake kwenye ukurasa wake, aliweka picha na video ya meli ikiondoka bandarini.

Golikipa wa Simba SC, Manula kupewa Tsh. Milioni 10 na RC Makonda

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar ea Salaam, Paul Makonda ameahidi kutoa zawadi ya Tsh. milioni 10 kwa Golipika wa Simba SC, Aishi Manula na Tsh. Milioni 1 kwa wachezaji wengine ambao hapo jana walishinda kwenye MO Simba Awards 2019.

Ripoti: Watoto wa sasa wana hali nzuri kuliko miaka 20 iliyopita

Image
Ripoti mpya iliyochapishwa wiki hili kuhusu hali ya watoto duniani inaonesha kuwa kuna hatua kubwa imepigwa katika afya, elimu na usalama kwa mataifa mengi katika kipindi cha miaka 20 iliyopita. Shirika la kimataifa la Save the Children linasema hali za watoto zimeboreshwa katika nchi 173 kati ya 176, huku Singapore ikiorodheshwa kuwa kinara wa kutoa huduma bora kwa watoto. Shirika hilo lisilo la kiserikali linakadiria kuwa watoto milioni 690 wamekuwa wakinyimwa haki kutokana na kuumwa, vifo, ndoa za utotoni, mimba za mapema, utapia mlo au kutopata elimu, idadi hii ikiwa ni chini kutoka watoto 970 mwaka 2000. Nchi za Sierra Leone, Rwanda na Ethiopia zinatajwa kama nchi ambazo kwa kiwango kikubwa zimepiga hatua kuboresha maisha ya watoto katika kipindi cha miongo miwili iliyopita. Kidunia, vifo vya watoto vimepungua na kuna watoto pungufu karibu milioni 49 waliodumaa, huku China na India zikirekodi kiwango cha chini zaidi kidunia. Nchi nyingine za Afrika Mashariki ukiondoa R

Waziri Lugola atoa miezi miwili kwa Shirika la uzalishaji mali Jeshi la Magereza

Image
Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola ameiagiza bodi mpya ya Shirika la uzalishaji mali la Jeshi la Magereza nchini, ndani ya miezi miwili ihakikishe maeneo yote yaliyochini ya miliki ya Jeshi hilo yamepimwa na kuwa na hati miliki pamoja na nyaraka zote. Sambamba na hilo bodi ihakikishe inakuja na mipango thabiti ya kuimarisha shirika hilo, ikiwa ni  pamoja na  Jeshi la Magereza linajitegemea kwa kila kitu bila kutegemea Serikali kuu. Waziri  Kangi  Lugola umetoa maagizo hayo  Jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa bodi ya Shirika la uzalishaji mali la jeshi la Magereza iliyoundwa kusimamia miradi yote iliyochini ya Shirika hilo ili iweze kuleta tija kwa Jeshi na jamii. Amesema bodi hiyo  ihakikishe ndani ya miezi miwili kwa kushirikiana na wataalamu ndani ya Jeshi hilo maeneo yote yanayomilikiwa na jeshi la magereza yawe yemepimwa na kuwa na hati miliki halali, kwa sababu kumekuwa na migogoro mingi katika  maeneo hayo kwa sababu hayana hati miliki na kushindwa kuendelezwa. “Ni