Posts

Showing posts from September, 2020

Ujerumani yaondowa vikwazo vya safari ilivyoweka kwa COVID-19

Image
  Hatimaye Ujerumani imeondosha marufuku yake ya safari kwa nchi zote ambazo hazipo kwenye Umoja wa Ulaya, huku kila dalili zikionesha kuwa wimbi jipya la maambukizo ya virusi vya corona linaanza tena barani Ulaya. Kufunguliwa huko upya kwa mipaka na viwanja vya ndege kuliamuliwa na baraza la mawaziri wiki tatu zilizopita, lakini utekelezaji wake umeanza Alkhamis ya leo. Mataifa 160 duniani yanafaidika na uamuzi huu. Hata hivyo, uamuzi huu unaanza kutekelezwa wakati idadi ya maambukizo mapya ya COVID-19 ikipanda barani Ulaya, huku wengi wakionya kwamba bara hili limo kwenye ukingo wa kutumbukia kwenye awamu ya pili ya janga la virusi vya corona.  Ujerumani ilitowa indhari ya safari kwa ulimwengu mzima mnamo mwezi Machi, wakati virusi hivyo vikisambaa kwa kasi kaskazini mwa Italia, lakini ikaiondosha kwa mataifa mengi ya Ulaya mwezi Juni.  Mwezi uliopita, Ujerumani ilianza tena kutangaza tahadhari kwa maeneo kadhaa ya Ulaya, baada ya maambukizo kuanza tena kupanda kwa watu 50 kati

Mama Samia ahitimisha ziara mkoani Manyara, aahidi kutatua Changamoto za Maji na Umeme

Image
Na John Walter-Hanang Mgombea Mwenza wa Urais wa Chama cha Mapinduzi Samia Hassan amesema endapo Chama cha Mapinduzi kitaendelea kuongoza katika miaka Mitano ijayo, watahakikisha changamoto zote za Maji na umeme zinamalizika. Samia Hassan ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  ametoa ahadi hizo wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya Hanang mkoani Manyara Septemba 30, 2020 katika kampeni za Chama hicho za kunadi ilani ya mwaka 2020-2025 iliyofanyika viwanja vya Shule ya Msingi Katesh A. Amesema serikali ya Ccm chini ya uongozi wa Rais John  Pombe Magufuli inayojali wanyonge itahakikisha suala la tatizo la Maji, Umeme na Miundo mbinu ya bara bara linamalizika  nchini. "Kwa hiyo mniamini kwamba maeneo yote ambayo hayana maji, maji yanakuja" alisema Samia. Ameongeza kuwa serikali ya Chama cha Mapinduzi  inakwenda kuifanyia kazi ahadi ya  kuweka kituo cha Afya kila kata na Zahanati kila kijiji ili kuwasogezea wananchi huduma karibu huku utarat

Siku ya wazee duniani: Jamii iwajibike kuwatunza

Image
  Oktoba 1 kila mwaka, ni Maadhimisho ya Siku ya Wazee Duniani inayotambulika na Umoja wa Mataifa katika Azimio namba 45/106 la mwaka 1990 - Siku hii ni mahususi kwa ajili ya kutambua Haki na Changamoto wanazokumbana nazo wazee katika jamii. Tanzania maadhimisho haya mwaka huu yatafanyika kimkoa - Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya, Naphtali Ng'ondi amesema Serikali imefanikiwa kupunguza mauaji ya wazee nchini kutoka wazee zaidi ya 500 miaka mitano iliyopita, na mwaka 2019 mauaji 74 tu yaliripotiwa - Aidha, amesema wameongeza idadi ya wazee wanaopatiwa Huduma za Afya bure na pia, wameboresha Vituo vya Kuwatunza Wazee nchini

Ditopile azidi kuibomoa CHADEMA, Awarudisha wanachama wao 26 CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kata

Image
Amsha amsha ya Mgombea Ubunge Viti Maalum Wanawake Mkoa wa Dodoma CCM, Mariam Ditopile kwenye uzinduzi wa kampeni za Udiwani Kata ya Mpamantwa wilayani Bahi zimefanikiwa kuwarudisha kwenye chama hicho wanachama 26 wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kata hiyo, Emmanuel Elias. Akizungumza katika uzinduzi huo ambao amemnadi Mgombea Urais wa CCM, Dk John Magufuli, Mgombea Ubunge Kenneth Nolo na Mgombea Udiwani Sosthenes Mpandu amesema Rais Magufuli mwaka 2015 alisema anataka kwenda kushughulika na shida za wananchi na kweli ametekeleza ahadi yake hiyo ambapo leo elimu ya msingi hadi kidato cha nne ni bila malipo wazazi hawalipi badala yake Serikali ya Dk Magufuli inalipa zaidi ya Sh Bilioni 24 kila mwezi ili watoto wakasome. " Magufuli alisema anaenda kujenga Hospitali kila Halmashauri au Wilaya, kwenye Hospitali zaidi ya 70 zilizojengwa Nchi nzima nyie watu wa Bahi mna Hospitali ambayo Dk Magufuli ameijenga kwa Sh Bilioni 1.7 sambamba na vifaa tiba vyake, amejenga vituo 484 N

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani akataliwa kuonana na Papa Francis

Image
 Vatican imemkatalia waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Mike Pompeo kuonana na Papa Francis. Kiongozi huyo wa juu wa Kanisa Katoliki ameelezwa kuwa hawapokei wanasiasa wakati wa kipindi cha uchaguzi. Hatua hiyo inaongeza hali ya mzozo wa kidiplomasia baada ya kauli ya Bwana Pompeo kuhusu China na Kanisa Katoliki. Vatican ilimshutumu Pompeo kuwa anajaribu kutumia suala hilo kuvutia wapiga kura wa uchaguzi wa urais wa mwezi Novemba nchini Marekani. Katika makala ya mwanzoni mwa mwezi Septemba, Bwana Pompeo alisema kanisa Katoliki linapoteza ''mamlaka yake ya kinidhamu'' kwa kufanya makubaliano mapya na China kuhusu uteuzi wa maaskofu. Donald Trump anapata uungwaji mkono kutoka kwa mashirika ya kidini ya kihafidhina, pamoja na wapiga kura wa Kikatoliki wa kihafidhina, ambao wengine wanadhani Papa Francis ni mtu mwenye uhuru sana. Makundi ya haki za binadamu yanasema kuwa Wakatoliki wengi nchini China wanateswa kwa kuahidi utii kwa Papa badala ya chama rasmi cha Wak

FC Bayern Munich yatwaa ubingwa wa German Super Cup

Image
Club ya FC Bayern Munich ya Ujerumani imefanikiwa kutwaa Ubingwa wa German Super Cup dhidi ya Borussia Dortmund katika mchezo wa fainali uliochezwa bila uwepo wa mashabiki viwanjani. Katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani wa hali ya juu umemalizika kwa FC Bayern Munich kupata ushindi wa magoli 3-2, magoli ya Bayern yakofungwa na Joshua Kimmich na Thomas Muller. Borussia Dortmund magoli yao mawili yalifungwa na Brandt na Haaland, ushindi huo sasa unamfanya Thomas Muller aandike rekodi ya kuwa mchezaji wa kijerumani mwenye mafanikio zaidi baada ta kutwaa taji lake la 27.

Tetesi za soka kimataifa

Image
 Manchester United imeanza mazungumzo na Barcelona kuhusu kumnyakua kwa mkopo mshambuliaji Mfaransa Ousmane Dembele 23. (Mirror) Tottenham wamemaliza makubaliano ya kumsajili mshambuliaji wa Benfica Carlos Vinicius,25, kwa mkopo, ambaye gharama ya kuondoka kwake ni kiasi cha pauni milioni 89 kwa mujibu wa kufungu cha mkataba wake. (Mail) Wakala wa mshambuliaji wa Real Madrid Luka Jovic,22, amesema raia huyo wa Serbia anataka kujiunga na Manchester United, huku inter Milan na Roma zikimtolea macho pia. (Star) Liverpool wanajiandaa kukubali ofa ya pauni milioni 23 kutoka Sheffield kwa ajili ya mshambuliaji Rhian Brewster. (Sun) Wekundu hao pia wamejiandaa kufaidika na kiungo wa zamani Philippe Coutinho wa Barcelona, ​​na kitita cha pauni milioni 4.4 ikiwa Mbrazili huyo,28 atacheza mechi nyingine 14. (Mirror) Manchester United wamekataa kuhusishwa kwao na taarifa za kumsajili Ainsley Maitland-Niles,23, ambaye anaweza kucheza nafasi ya ulinzi na kiungo wa kati kutoka Arsenal. (Manche

MAGAZETI YA LEO 1/10/2020

Image
 

Mujata yaonya uvunjifu wa amani kuelekea uchaguzi mkuu

Image
  Na Amiri Kilagalila,Njombe Shirika la muungano wa jamii Tanzania(MUJATA) limeitaka jamii ya Tanzania kutunza amani iliyopo nchini hasa kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika 28 oktoba mwaka huu. Hayo yalisemwa na katibu mkuu wa shirika hilo ngazi ya Taifa Hekima Malila wakati wa kikao cha shirika hilo ngazi ya kanda uliofanyika katika mkoa wa Njombe na kushirikisha wajumbe kutoka nyanda za juu kusini. Alisema jamii inapaswa kutambua kuwa amani iliyopo hapa nchini imeenziwa kwa muda mmrefu na waasisi wa nchi hii na kutuachia ambapo mpaka sasa imeendelea kuwepo. Alisema jamii inapaswa kutambua kuwa amani iliyoopo nchini haikununuliwa popote pale hivyo endapo jamii itaruhusu ipotee itatugharimu katika kuirudisha amani hiyo. "Tumezoea kuona tunaishi kwa amani , tunaabudu kwa amani na hata kazi zetu za maendeleo zimekuwa zikiendelea na nchi yetu kuelekea uchumi wa kati kwasababu kuna amani" Alisema Hekima. Alisema jamii inapaswa kutambua kuwa yenyewe ina

Sumaye aishukia Vikali CHADEMA, asema hawawezi kuongoza nchi

Image
  Na John Walter-Hydom, Mbulu Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Frederick Sumaye amesema vyama vya Upinzani nchini haviwezi kuongoza nchi kwa sababu hawana sera. Ameyasema hayo Leo septemba 30,2020 akizungumza na wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini katika mkutano wa Mgombea Mwenza Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia  Suluhu Hassan kunadi Sera za  Chama cha Mapinduzi katika viwanja Vya Haydom. Sumaye amesema Chama alichotoka  CHADEMA,  ni Chama cha Uwana harakati na hakina sera  zozote za kuwasaidia wananchi. 'CHADEMA wanafikiri kuwa nchi ya Tanzania bado ipo  mikononi mwa  Wakoloni, wanapiga kelele utafikiri bado tunatawaliwa' alisema Sumaye 'Nilienda kule  lakini baada ya kugundua hawana chochote nikaamua kurejea nyumbani' alisisitiza Sumaye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Manyara Simon Lulu amesema Chama hicho kinajiandaa kwa ushindi wa kishindo kwa sababu kimefanya maendeleo kwa wananchi. Amemweleza Mgombea Mw

Vijiji 73 Kati Ya 77 Misenyi Vyapatiwa Umeme

Image
  VIJIJI 77 kati ya vijiji 73 vya wilaya ya Missenyi mkoani Kagera vimepelekewa huduma ya umeme na vijiji 4 bado havina umeme. Hayo yamesemwa jana (Jumanne, Septemba 29, 2020) na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Kassambya, katika mikutano uliofanyika kwenye uwanja wa Mashujaa, wilayani Missenyi, mkoani Kagera. Amevitaja vijiji ambavyo havina umeme na vipo kwenye mpango wa kupelekewa umeme kuwa ni vijiji vya Buchurago, Katano, Kakunyu na Bugango. Akizungmzia sekta ya mifugo ambayo imetajwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020 hadi 2025 kuanzia ukurasa 47-52, Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imeisimamia vizuri sekta ya mifugo ili kuhakikisha wafugaji wanapata manufaa. “Shilingi milioni 23 zimetumika kukarabati machinjio ya Bunazi hapa Misenyi, pia tumerahisisha uuzaji wa mazao ya mifugo kwa kufuta tozo kero 114 katika sekta ya kilimo, mifugo na uvu

Guinea 'imefunga mipaka' na majirani zake kabla ya uchaguzi

Image
  Guinea imefunga mipaka yake na Senegal na Guinea-Bissau kabla ya uchaguzi mkuu, afisa wa serikali amenukuliwa na shirika la habari la AFP. Afisa huyo alisema hatua hiyo imechukuliwa kutokana na sababu za kiusalama kwa mujibu wa shirika hilo. Waziri wa usalama wa ndani Guinea-Bissau, Botche Cande, amesema mpaka huo umefungwa tangu siku ya Jumapili lakini mwezake wa Guinea hajathibitisha hilo. Rais wa Guinea Alpha Condé anagombea muhula wa tatu madarakani katika uchaguzi mkuu wa Oktoba tarehe 18, hatua ambayo imezua utata.

Magufuli aahidi upanuzi bandari ya Manda wilayani Ludewa-Njombe

Image
  Na Amiri Kilagalila,Njombe Chama cha mapinduzi CCM kupitia kwa mgombea wao wa nafasi ya,Rais ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt  John Pombe Magufuli,wameahidi kupanua bandari ya Manda wilayani Ludewa mkoani Njombe ili kurahisisha usafiri kwenye ziwa Nyasa. Magufuli ameyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni zake mjini Makambako wakati akizungumzia utekelezaji wa Ilani ya Chama hicho kwa mwaka 2015-2020 na namna watakavyotekeleza Ilani yao 2020-2025 "Tumepanga kupanua bandari ya Manda iliyopo wilaya ya Ludewa ili kurahisisha usafiri katika ziwa Nyasa kama mnavyofahamu kwenye miaka mitano iliyopita tumejenga Meli mpya tatu kwenye ziwa Nyasa kwa ghalama ya shilingi bilioni 20.4 tunataka ziwe zinatua mpaka Manda kwenye Bandari" alisema Magufuli. Vile vile amesema wako mbioni kukamilisha ujenzi wa Chuo cha Ufundi (VETA) kinachojengwa Shaurimoyo wilayani Ludewa mkoani humo ili kuwezesha vijana kupata mafunzo ya ufundi waweze kujiajili na kuajiliwa.

Hospitali Ya Wilaya Karagwe Yakamilika Kwa 98%

Image
 SERIKALI ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imetumia sh. bilioni 1.8 kujenga majengo mbalimbali ya hospitali ya wilaya ya Karagwe ambayo yamekamilika kwa asilimia 98. Hayo yamesemwa jana (Jumanne, Septemba 29, 2020) na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wakazi wa kata ya Kayanga, katika mikutano uliofanyika kwenye uwanja wa Changarawe, wilayani Karagwe, mkoani Kagera wakati . Akielezea ujenzi wa vituo vya afya kwenye wilaya hiyo, Mheshimiwa Majaliwa alisema sh. milioni 900 zimetumika kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya vituo cha afya ambapo kati ya hizo, sh. milioni 500 zimetumika wa majengo ya kituo cha afya cha Kayanga ambapo kituo hicho kimekamilika na kinatoa huduma. “Shilingi milioni 400 zimetumika kwa ujenzi wa majengo ya kituo cha afya cha Nyakayanja na ujenzi umekamilika. Pia shilingi bilioni 2.5 zimetumika kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi huku fe

Armenia yakataa upatanishi wa Urusi katika mzozo na Azerbaijan

Image
  Armenia imekataa upatanishi wa Urusi katika mzozo wake na Azerbaijan juu ya jimbo la Nagorny Karabakh, huku mapigano makali yakiendelea kwa siku ya nne. Armenia Jumatano imekataa pendekezo la Urusi la kutaka kuwa mpatanishi katika mazungumzo ya amani na hasimu wake mkubwa Azerbaijan, huku mapigano yakiwa yanaendelea kupamba moto kwa siku ya nne katika jimbo linalotaka kujitenga la Nagorno Karabakh. Waziri mkuu  wa  Armenia Nikol Pashinyan amesema haitakuwa sahihi kufanya mazungumzo ya  amani  na Azerbaijan chini ya upatanishi wa  Urusi, wakati mapigano ya kuwania udhibiti wa jimbo yakiwa yanaendelea. "Sio sahihi kabisa kuzungumzia kuhusu mkutano kati ya  Armenia, Azerbaijan na Urusi  katika wakati wa uhasama mkubwa," amesema Pashinyan wakati akizungumza na shirika la habari la Urusi Interfax. Ameongeza kuwa hali endelevu na mazingira yanahitajika kwa ajili ya mazungumzo hayo.  Vyombo vya habari nchini Urusi vimeripoti Jumatano kuwa waziri mkuu Pashinya amesema A

Mahakama kuamua uhalali wa Museveni kugombea tena urais

Image
  Mahakama ya Haki ya Afrika Mashaki inatarajiwa kuamua kesi inayopinga uhalali wa Yoweri Museveni kugombea tena urais wa Uganda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2021. Mahakama ya juu zaidi ya Uganda iliidhinisha marekebisho ya katiba ili kuondoa ukomo wa miaka kwa wagombea wa urais. Marekebisho ya katiba ya mwaka 2017 iliondoa kifungu cha sheria kinachowataka wagombea uraisi kuwa na umri wa chini ya miaka 75. Hatua hiyo ilimruhusu rais Yoweri Museveni, ambaye ana umri wa miaka 75, kugombea mhula wa sita katika uchaguzi wa Januari mwaka 2021. Amekuwa madarakani tangu mwaka 1986. Wakili Male Mabirizi aliwasilisha shauri katika mahakama ya Afrika Mashariki, iliyopo nchi jirani ya Tanzania, kupinga uamuzi wa Mahakama ya Juu Zaidi ya Uganda. Anataka kifungu cha ukomo wa miaka wa wagombea urais kilichotolewa katika katiba kirudishwe. Katika nyaraka alizowasilisha mahakamani alisema marekebisho hayo ya katiba yalifanywa "katika mazingira ya vurugu baada ya jeshi la polisi kupel

Mdahalo wa Urais: Ukweli wa madai ya Trump na Biden

Image
  Rais Trump na mpinzani wake wa chama cha Democratic Joe Biden wamekabiliana kwa mara ya kwanza katika mdahalo wa kwanza kati ya mitatu itakayopeperushwa kwa njia ya televisheni kabla ya uchaguzi wa urais utakaofanyika Novemba. Wakati wa mdahalo huo uliochukua dakika 90, wagombea hao walikabiliana kwa kila jambo walilokuwa wanazungumzia kuanzia uchumi hadi namna ya kukabiliana na janga la virusi vya corona. Kitengo cha Reality Check BBC kimechambua baadhi ya madai hayo. Trump: "Tumeimarisha uchumi kwa kiasi kikubwa katika historia" Uamuzi: Huo sio ukweli - kumekuwa na wakati katika historia ya Marekani ambapo uchumi umeimarika zaidi. Kabla ya mlipuko wa virusi vya corona, rais Trump alidai kwamba uchumi umeimarika kuliko kipindi kingine chochote kile. Ni kweli uchumi ulikuwa unafanya vizuri kabla ya janga la corona - ikiwa ni kile kilichokuwa kinaendelea wakati wa utawala wa Obama - lakini kuna wakati ambapo uchumi uliimarika zaidi. Biden: "Tuna asilimia 4

NEC: Kosa kubandika bango kwenye nyumba za watu

Image
  Mkurugenzi Msaidizi wa Elimu ya Mpiga Kura, kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Monica Mnanka, amesema kuwa mabango yote ya wagombea yanayopandikwa kwenye nyumba ya mtu lazima wahusika wawe wameridhia vinginevyo itakuwa ni kosa na mhusika ana haki ya kuyaondoa. Akizungumza leo kwenye mahojiano katika kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio Mnanka amesema kuwa yapo maeneo ambayo mabango ya wagombea yanaweza kuwekwa kwa mujibu wa sheria. “Kama bango umeweka kwenye nyumba ya mtu awe ameridhia kama hajaridhia hilo ni kosa, na pia kubandua bango la mgombea katika sehemu iliyoruhusiwa kwa mujibu wa sheria faini yake si chini ya shilingi elfu thelathini, “ alisema Mnanka. Aidha, Mnanka amesisitiza kuwa Mtanzania yeyote ambaye ni mpiga kura haruhisiwi kuharibu mabango ya mgombea yeyote kwani kila mgombea ana nafasi ya kunadi sera zake katika kipindi chote cha kampeni. "Mpiga kura anatakiwa asiharibu mabango ya vyama au mgombea mwingine hatakama hukipendi kwa sababu

Viongozi wa Azerbaijan na Armenia wakataa kuzungumza

Image
Viongozi wa Azerbaijan na Armenia wamepuuzia pendekezo la mazungumzo ya amani baina yao, huku kila mmoja akimshutumu mwengine kwa kuzuwia mapatano juu ya jimbo linalowaniwa la Nagorno-Karabakh, ambako watu kadhaa wameshauawa na kujeruhiwa ndani ya kipindi cha siku tatu za mapigano makali.  Katika tukio la karibuni kabisa, Arnmenia imesema ndege yake moja ya kijeshi iliangushwa na ndege nyengine ya kijeshi ya Uturuki, ambayo ni mshirika mkubwa wa Azerbaijan, na kumuua rubani wake.  Uturuki na Azerbaijan zimekanusha taarifa hiyo. Jumuiya ya kimataifa inazitaka pande hizo mbili kufanya mazungumzo ya kukomesha mzozo huo wa miongo kadhaa baina ya mataifa hayo yaliyowahi kuwa sehemu ya Shirikisho la Jamhuri za Kisovieti kwenye Milima ya Caucasus.  Nagorno-Karabakh inatambuliwa kimataifa kuwa sehemu ya Azerbaijan, lakini imekuwa chini ya udhibiti wa vikosi vya waasi wanaoungwa mkono na Armenia tangu mwaka 1994.  Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa jana lilitoa tamko linazozitaka pa

Lissu adai bado hajapokea wito wa malalamiko

Image
Mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amesema kuwa hadi sasa bado hajapokea wito wala malalamiko yoyote kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kama taarifa ya tume hiyo ilivyoeleza hapo jana. Lissu ametoa kauli hiyo hii leo Septemba 30, 2020, wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha, na na kusisitiza kuwa kwa sababu hana wito wowote yeye ataendelea na ratiba zake za kampeni kama ilivyo kwenye ratiba. "Kama kweli mimi ni mlalamikiwa, kanuni za maadili zinasema mlalamikiwa aandikiwe malalamiko na akabidhiwe na yeye ndiye anayetakiwa kuitwa, hadi hapa niliposimama tangu mmeanza kusikia mimi kuitwa kwenye kamati ya maadili, sijaona afisa yoyote wa tume akinifuata kuniletea malalamiko yoyote kwa maandishi na wito wowote,” alisema Lissu. Aidha, Lissu amedai kwamba Watanzania wapo tayari kuipigia kura CHADEMA kwenye nafasi ya urais, ubunge na udiwani na kila mahali ambako amekwenda amepokelewa na amehutubia mikutano ya mael

Imarati yatetea kuanzisha mahusiano rasmi na Israel

Image
  Umoja wa Falme za Kiarabu umetetea uamuzi wake wa kuanzisha mahusiano rasmi na Israel na kukosowa kile ulichosema ni uingiliaji kati kwa mambo ya Waarabu unaofanywa na mataifa ya kigeni, akizilenga Iran na Uturuki.  Kwenye hotuba yake mbele kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Imarati, Sheikh Abdullah bin Zayed Al Nahyan, alidai kwamba uamuzi wa nchi yake uliotangazwa mwezi Agosti uliuzuwia mpango wa Israel kuyanyakuwa maeneo zaidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi.  Hata hivyo, Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amenukuliwa mara kadhaa akisema mpango huo umesitishwa kwa muda tu.  Al Nahyan aliliambia baraza hilo hapo jana kwamba Imarati inatarajia kuwa Wapalestina na Waisraili watatumia fursa hiyo kurejea kwenye meza ya mazungumzo kwa ajili ya amani ya wote na ya kudumu.  Wapalestina wamezikosowa Imarati na Bahrain kwa kusaini makubaliano na Israel chini ya ushawishi wa Marekani, wakisema ni kitendo cha usaliti.

Maziwa matatu yaliojificha yagunduliwa katika sayari ya Mars

Image
  Maziwa matatu ya chini ya ardhi yamegunduliwa karibu na eneo la kusini mwa sayari ya Mars. Wanasayansi pia wamethibitisha uwepo wa ziwa la nne - ambalo ishara za uwepo wake uligunduliwa 2018. Maji ni muhimu kwa baiolojia, hivyobasi ugunduzi huo utakuwa muhimu kwa watafiti wanaotafuta uhai nje ya dunia. Lakini maziwa hayo pia yamedaiwa kuwa na chumvi nyingi sana hali inayofanya kiumbe chochote kutoweza kuishi ndani yake. Hali nyembemba ya hewa katika sayari ya Mars ina maana kwamba uwepo wa maji katika sakafu ya sayari huo upo chini . lakini maji yanaweza kuwepo chini ya ardhi yake. Ugunduzi huo wa hivi karibuni ulifanyika kwa kutumia data kutoka kwa kifaa cha rada katika kituo cha angani cha bara Ulaya Esa ambacho kimekuwa kikizunguka katika sayari hiyo nyekundu tangu 2003. Mwaka 2018, watafiti walitumia data kutoka rada ya Mars ili kuripoti ishara za ziwa lenye ukubwa wa kilomita 20 ndani ya ardhi ya Mars . Hatahivyo ugunduzi huo unatokana na tafiti 29 zilizofanywa na

Tembo 30 wa Zimbabwe 'waliuawa na bakteria

Image
  Maafisa wa wanyamapori nchini Zimbabwe wanashuku ugonjwa wa bakteria unaofahamika kama haemorrhagic septicaemia ndio chanzo cha vifo vya zaidi ya tembo 30 mwisho wa mwezi Agosti. Sampuli zimetumwa ili kufanyiwa uchunguzi zaidi. Tembo hao walipatikana wakiwa wamelala kifudifudi, hali ambayo wataalamu wanaashiria walikufa ghafla. Wasimamizi wa mbuga za wanyama hawaamini waliuawa na wawindaji haramu, kwa sababu hawakutolewa pembe zao.

Wakazi wa eneo la Mkunwa kurasimishiwa maeneo yao

Image
  Na Faruku Ngonyani, Mtwara. Timu ya Wataalamu wa ardhi kutoka Halmashsuri ya Wilaya ya Mtwara wameanza rasmi mchakato wa upimaji eneo la Mkunwa ambao kwa Sasa ni Makao Makuu ya Halmashauri hiyo. Zozi la Upimaji wa eneo hilo  likiwa na lengo la kurasimisha makazi ya wananchi  sambamba na kuupanga mji huo wa Mkunwa. Kwa upande wa wananchi wamefurahishwa na zoezi hilo ambapo mara baada ya  kumalizika kwa zoezo la Urasimishaji wa mji huo  kutawawezesha wananchi kutambua na kujua mipaka ya maeneo wanayoishi. Kata ya Mkunwa ipo katika Mpango wa Mji kabambe wa Mtwara (Mtwara Master Plan) ambapo kuanza kwa  zoezi hilo ni maandalizi katika kuendelea kutekeleza Mpango huo Kimkakati Mkoani Mtwara

Mahakama yasitisha mgomo katika hospitali kubwa zaidi Afrika Mashariki

Image
  Mahakama ya wafanyakazi nchini Kenya imesitisha mgomo wa uliyoitishwa na wafanyakazi wa hospitali Kuu ya Kenyatta, KNH. Jaji Maureen Onyango ameagiza zaidi ya wafanyakazi 5,000 kurejea kazini wakisubiri kusikizwa kwa kesi. Muungano wa wafanyakazi unaowawakilisa wauguzi, madaktari na wafanya kazi wengine katika hospitali hiyo umeagizwa kufika mbele ya mahakama hiyo Oktoba tarehe 6. Wafanyakazi wanalalamikia kucheleweshwa kwa malipo yao ya mishahara na marupurupu yaliyoboreshwa.

KIWANJA KINAUZWA DODOMA

Image
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X 30 ). Kiwanja ni kizuri sana watu wameshaanza kujenga na wengine washa hamia, Umeme na Maji vyote vipo.  kutoka njiapanda ya Nkuhungu ni KM 3 mpaka kwenye kiwanja..  Bei Million 3,500,000 Piga simu 0719788949 MAJIRANI WAKO .

Mama Samia apokelewa na Mafuriko ya watu Mbulu Mjini

Image
  Na John Walter-Mbulu  Mgombea Mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ambae pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika mwendelezo wa Kampeni za kumuombea mgombea Urais wa Chama hicho Ndugu John Magufuli, Madiwani na Wabunge wa Ccm  katika mkoa wa Manyara amepokelewa kwa Shangwe na Maelfu ya wananchi wa Jimbo la Mbulu mjini huku wakiahidi kukipigia kura chama hicho ifikapo Oktoba 28 mwaka huu. Akizungumza na Wananchi hao Samia amesema serikali imefanya mengi katika Jimbo la Mbulu Mji kwenye Sekta ya Afya,Elimu na Miundombinu ya bara bara ambapo kwa sasa inakwenda kutekeleza Ujenzi wa bara bara kutoka Karatu-Mbulu-Hydom mpaka Singida Kilomita 190 baada ya kufanya upembuzi yakinifu. Samia amesema ujenzi wa bara bara hiyo utaanza muda wowote kwa kilomita 50 awamu ya kwanza. Ameongeza kuwa bara bara ya Mbulu hadi Mbuyu wa Mjerumani kilomita 63 upembuzi yakinifu unakamilika na

Jamshid bin Abdullah Al Said: Fahamu aliko Sultani wa mwisho wa Zanzibar

Image
  Baada ya kuishi mafichoni hususan nchini Uingereza Jamshid bin Abdullah Al Said, aliyekuwa sultani wa Zanzibar , akiwa ndio Sultan wa mwisho wa mssultani waliotawala miaka 91 kisiwani humo kutoka kwa familia ya al Busaid , alihamia katika ufalme wa Oman. Mtu huyu ambaye aliitawala Zanzibar hadi alipoondolewa katika mapinduzi ya mwezi Januari 1964 aliwasili mjini Muscat hivi karibuni. Gazeti la The Guardian linasema kwamba serikali ya Oman ilikataa maombi kadhaa yaliotolewa na Sultan huyo ili kumruhusu kuishi katika ufalme huo. Lakini ndugu yake mmoja mjini Muscat aliambia gazeti la The National mjini Abu Dhabi kwamba ombi lake la kutaka kuishi Oman limekubalika kutokana na umri wake. Amekua akitaka kuishi siku zake za mwisho katika taifa hilo la mababau zake ''na sasa anafurahia kuweza kufanya hivyo'', aliongezea. Afisa mmoja wa serikali alikataa kutoa tamko lake kulingana na gazeti la The Guardian. Uhuru na mapinduzi Jamshid bin Abdullah alizaliwa tar