Katika kuelekea kwenye uchaguzi mkuu ujao ,Chama Cha Mapinduzi (CCM),mjini Kibaha kimeanza kuwachukulia hatua baadhi ya wapambe wa wagombea ,wanaojipitisha kuwapigia debe wenye nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi . Aidha chama hicho kimepiga marufuku wagombea wanaojipitisha na wapambe wao ,kuacha mara moja kufanya hivyo kwani wanakiuka taratibu na maadili ya chama. Akitoa taarifa kuhusiana na mkutano mkuu wa jimbo ,unaotarajia kufanyika march 2 mwaka huu,mjini Kibaha ,kwa lengo la mbunge wa jimbo hilo Silvestry Koka kueleza utekelezaji wa ilani, katibu wa CCM Kibaha Mjini ,Afidh Luambano alisema ,hadi sasa wamekaa vikao na kuwaonya wale waliosikika kujipitisha kuwanadi wagombea wao. “Hizo ni vurugu ,waache madiwani na mbunge aliyepo madarakani wafanye kazi na kumaliza muda wake ,waache kujipenyeza penyeza kwasasa sio muda wao”alifafanua Luambano. Luambano alieleza ,chama hicho kitaendelea kusimamia msingi na haki na wamejipanga kushinda kata zote na jimbo na Rais kati...