Posts

CHUO CHA TUMAINI JIPYA IRINGA KINATANGAZA NAFASI ZA MASOMO

Image
    Mkuu wa chuo cha afya na sayansi chirikishi tumaini jipya kilichopo  mafinga mjini mkoani iringa  chenye usajili wa baraza la taifa elimu ya ufundi nacte no hs/ 144 anawatangazia nafasi za masomo kwa mwaka  wa masaomo 2020/2021 kwa  kozi  zifuatazo Ordinary diploma in clinical medicine(  clinical officer) miaka mitatu technician certificate in clinical medicine(clinical assisstance)miaka miwili.           Mwombaji awe ufaulu wa alama ( D ) kwa masomo ya fizikia chemia na biologia Ordinary diploma in clinical medicine upgrading  ( mwaka moja) sifa awe amemaliza na kufaulu technician certificate in clinical medicine.    Pia chuo kina nafasi za kuhamia mwaka wa masomo 2020/2021, kwa wanafunzi wa  mwaka wa pili na mwaka wa tatu Maombi hufanyika chuoni kwa idhini ya nacte kwa mawasiliano fika chuoni tumaini jipya au piga simu  0756916610 / 0764986544 / 0762251717 Chuo kina mazingiza tu...

Kampuni 21 za nunua korosho RUNALI, bosi wa CBT na DC watema cheche

Image
Na Ahmad Mmow, Lindi.   Kampuni 21 zimenunua kilo 2,854,008 za korosho katika chama kikuu cha ushirika cha RUNALI, kupitia mnada wa kwanza kwa msimu wa 2020/2021 uliofanyika kwenye viwanja vya ofisi kuu ya chama cha RUNALI iliyopo mjini Nachingwea.  Katika mnada huo ambao ulikuwa tofauti na minada ya misimu iliyopita kwa korosho kununuliwa kwa mifumo miwili tofauti ( mtandao kupitia soko la bidhaa,TMX na barua za kawaida ndani ya boksi la zabuni) ilishuhudiwa bei 82 tofauti zilizoombewa na kampuni hizo kununua zao hilo.  Ambapo kampuni zilizofanikiwa zimenunua kwa bei ya juu ya shilingi 2,555 na bei ya chini shilingi 2,422 kwa kila kilo moja.   Korosho zilizonunuliwa zipo katika maghala  yaliyopo katika wilaya za  Nachingwea na Ruangwa. Ambapo katika  ghala la Lipande, wilayani Ruangwa ambalo korosho zake zilinunuliwa kwa bei ya shilingi 2,395 hadi 2,345 lina kilo 580363.   Katika ghala Lindi farmes lililopo wilayani Nachingwe...

Borell: EU ina wasiwasi na mapigano mapya ya Nagorono Karabakh

Image
Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Josep Borell ameelezea wasiwasi wake kuhusiana na ripoti za ukiukaji makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya mataifa jirani yaliyo hasimu ya Armenia na Azerbaijan ya kuwania udhibiti wa jimbo la Nagorno Karabakh. Taarifa iliyotolewa na mwanadiplomasia huyo wa Umoja wa Ulaya, imesema kanda hiyo inatiwa shaka na operesheni za kijeshi zinazoendelea ikiwemo zinazohujumu maeneo ya makaazi na kuwalenga raia. Taarifa hiyo Borell imetolewa baada ya kuvunjika kwa sehemu fulani makubaliano ya kusitisha mapigano kufuatia kuzuka makabiliano mapya huku kila upande ukiulaumu mwingine kuhusiana na kilichotokea. Borell amesema Umoja wa Ulaya unatoa wito wa pande hasimu kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano na kuanza mazungumzo chini ya upatanishi wa kundi liitwalo OSCE Minsk linaloongoza juhudi za kumaliza mzozo wa Karabakh.

LA Lakers Bingwa wa NBA 2020, LeBron ang’aa tena

Image
Staa wa LA Lakers LeBron James leo ameshinda taji la NBA 2020, Lebron anakuwa kashinda mataji manne ya NBA akiwa na timu tatu tofauti. LeBron akiwa ndio kwanza ana umri wa miaka 35, ameshinda taji hilo akiwa na vilabu vya Miami Heat 2, Cleveland Cavaliers 1 na LA Lakers mara 1. Baada ya Ubingwa huo wa LA Lakers leo dhidi ya Miami Heats katika game 6 ya NBA, umemfanya LeBron kupewa tuzo ya MVP ya mchezaji mwenye thamani zaidi katika fainali za NBA baada ya kushinda Ubingwa 2012, 2013, 2016 na 2020.

Uingereza na Kenya kukusanya $ 5bn kufadhili elimu baada ya Covid-19

Image
Waziri Mkuu wa Uingereza na Boris Johnson na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wanatarajiwa kuzindua mpango utakaosaidia kukusanyadola bilioni tano sawa na (£3.8bn) kwa ajili ya kuwasomesha watoto kutoka jamii masikini duniani Idadi ya wanafunzi walioacha shule imeongezeka zaidi wakati wa janga la Covid-19. Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, Sayansi na utamaduni (Unesco) linakadiria kuwa hadi wanafunzi bilioni 1.3 duniani billioni wameacha shule huku wataalamu wakionya kuwa baadhi yao huenda wasirudi kutokana na hali ya kiuchumi ya nchi zao. Viongozi hao wawili pia watatangaza mpango wa kuandaa kwa pamoja kongamano kuu la elimunchini Uingereza katikati yam waka ujao kutafuta ungwaja mkono. Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson na Rais Uhuru Kenyatta watawashawishi viongozi kuhakikisha wanaenda shulewa kuwekeza zaidi katika mpango huo unaofahamika kama Global Partnership for Education.

Mwalimu mstaafu alivyonusurika kutapeliwa Milioni 7

Image
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Geita imefanikiwa kumrejeshea kiasi cha Sh. Mil tano na laki tano, Mwalimu mstaafu Adela Faustine, ambazo zilichukuliwa na mfanyabiashara Isack Nyamhanga wa Wilayani Chato. Akizungumzia tukio hilo Mkuu wa TAKUKURU mkoani Geita Leonidas Felix amesema mfanyabiashara huyo alimkopesha mwalimu  Adela, kiasi cha shilingi za Kitanzania laki saba na  kumlazimisha kurejesha milioni saba baada ya kugundua kuwa mwalimu huyo amelipwa kiinua mgongo baada ya kustaafu. ‘’Tulifanya upekuzi kwa huyu mtuhumiwa na alikutwa na kadi 64 za benki za wateja wake ambao ni wakopaji’’, amesema Leonidas Felix. Aidha mkuu huyo amesema mfanyabiashara huyo alitumia njia za vitisho ambapo alimtaka kulipa milioni saba ambayo ni sawa na asilimia 900 ambapo amesema hiyo ni dhuluma na kwamba TAKUKURU haitavumilia vitendo hivyo. Baada ya kutoa Milioni tano na laki tano katika awamu ya kwanza, mfanyabiashara huyo atamalizia milioni moja na laki tano...

EU ina wasiwasi na hatma ya usitishaji mapigano Nagorno Karabakh

Image
Umoja wa Ulaya umeelezea wasiwasi wake kuhusiana na ripoti za ukiukaji makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya mataifa jirani yaliyo hasimu ya Armenia na Azerbaijan yanayowania udhibiti wa jimbo la Nagorno Karabakh Taarifa iliyotolewa na mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Jossep Borell, imesema kanda hiyo inatiwa shaka na operesheni za kijeshi zinazoendelea ikiwemo zinazohujumu maeneo ya makaazi na kuwalenga raia. Taarifa hiyo Borell imetolewa baada ya kuvunjika kwa sehemu fulani makubaliano ya kusitisha mapigano baada ya kuzuka upya kwa makabiliano huku kila upande ukiulaumu mwingine kuhusiana na kilichotokea. Borell amesema Umoja wa Ulaya unatoa wito kwa Armenia na Azerbaijan kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano na kuanza mazungumzo chini ya upatanishi wa kundi  liitwalo OSCE Minsk linaloongoza juhudi za kumaliza mzozo wa Karabakh. Pande hizo mbili zilifikia makubaliano ya kusitisha mapigano, kubadilishana wafungwa na miili ya wale waliouwawa katika mapambano ...