Mikutano ya kampeni za mgombea Ubunge -Ludewa yatoa majibu ya kero ya Barabara iliyodumu kwa muda mrefu
Na Amiri Kikagalila, Njombe. Mbunge wa Jimbo la Ludewa aliyepita bila kupingwa kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) wakili Msomi Joseph Kamonga ameendelea na mikutano ya kampeni za Kumuombea kura Rais Dkt John Pombe Magufuli na madiwani wa CCM ikiwa zimebaki Siku 16 kuelekea Kufanyika kwa Uchaguzi mkuu nchini Tanzania hapo Oktoba 28, 2020. Kamonga akiwa katika kata ya Madilu wilayani Ludewa amewashukuru Wananchi wa eneo hilo kwa kukiamini Chama cha Mapinduzi na kumpitisha yeye bila kupingwa kuwa mbunge wa jimbo la Ludewa na amewaahidi kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabiri ikiwemo swala la Barabara. ''Ndugu zangu nimekuja kusema Asante sana,Jambo la pili nimekuja kuwaombea kura viongozi wa CCM, Tumekuja kumuombea kura Rais wetu Mpendwa Dkt,John Pombe Magufuli,tunamuombea kura Magufuli kwa ujasiri kutokana na mambo makubwa aliyoyafanya kwenye taifa letu ni Rais wa kipekee mfano pekee mwaka jana aliweka utaratibu wa Kusikiliza Changamoto za wafanyabishara mbalim...