Mchimbaji mdogo wa Madini ya Almasi wilaya ya Kishapu aibuka na Almasi Kubwa kuliko zote Tanzania. Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ametoa wito kwa wanunuzi wa Almasi kufika mkoani humo.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Zainabu Telack ndiye ameitangaza Almasi hiyo mbele ya waandishi wa habari kuwa inauzito wa karati 521 kuliko zote zilizochimbwa Mkoa wa Shinyanga au Tanzania kwa kuwa hadi sasa Almasi zenye uzito wa karati 300-421ambazo zimekuwa zikipatikana mgodi wa wiliamson- Mwadui uliopo wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.
Picha na StarTV
Comments
Post a Comment