Posts

Kamishna Mkuu TRA awapa neno wajumbe wa EARATC kuhusu maadili

Image
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dkt. Edwin Mhede amesema kuwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hazina budi kutilia mkazo suala la maadili ili kujenga uelewa wa pamoja na kuwa na mikakati shirikishi ya kutokomeza vitendo viovu vinavyofanywa na baadhi ya watumishi wa mamlaka za mapato vinavyokwamisha ukusanyaji mzuri wa mapato. Dkt. Mhede ameeleza hayo wakati akifungua mkutano wa 10 wa Mamlaka za Mapato Afrika Mashariki (EARATC) kuhusu maadili unaoendelea Jijini Dodoma. Amefafanua kwamba, katika mkutano huo masuala mbalimbali yanajadiliwa zikiwemo fursa mbalimbali pamoja na changamoto kama vile masuala ya upitishaji wa mapato haramu mipakani pamoja na namna ya kushirikiana katika kutoa adhabu kwa wafanyaji makosa hayo. “Katika mkutano huu tunajadili masuala mbalimbali, mfano suala la maadili kama vile utovu wa nidhamu kwa watumishi wetu wa mamlaka za mapato, lakini pia tutaona namna ya kushirikishana katika kutoa adhabu kwa wafanyaji makosa katika ...

Waziri Mpina atangaza neema kubwa kwa Wafugaji

Image
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amezindua kampeni ya kitaifa ya uogeshaji mifugo nchini na kutangaza neema kubwa kwa wafugaji ambapo sasa ng’ombe mmoja ataogeshwa kwa shilingi 50 badala ya sh 500 huku Mbuzi na Kondoo wakiogeshwa kwa sh 10 kila mmoja. Uamuzi huu wa Serikali utawawezesha kuokoa shilingi bilioni 19 ambazo wafugaji wangezitumia kuogesha mifugo yao lakini ambapo sasa itatumika shilingi bilioni 2.16 tu huku Serikali ikiwapatia wafugaji ruzuku ya asilimia 90 ambapo kama wafugaji wangeendelea na bei hiyo ya miaka ya nyuma wangelazimika kutumia sh bilioni 21.6. Akizungumza mara baada ya uzinduzi wa Kampeni ya uogeshaji mifugo awamu ya pili katika Josho la Kikonko wilayani Mlele na baadae mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Majimoto, Waziri Mpina alisema kupitia  mpango huo Serikali itasambaza dawa ya ruzuku lita 12, 546 kwenye majosho yanayofanya kazi 1,733 nchini kote. Huku Mvua kubwa ikinyesha kwenye mkutano huo, Waziri Mpina alitumia zaidi ya...

Wananchi wa Kisarawe wahakikishiwa huduma ya Maji ndani ya siku tatu

Image
Kufikia mapema wiki ijayo, Wakazi wa mji mdogo wa Kisarawe wanaondoka na na adha ya maji ya muda mrefu baada ya ujenzi wa mradi wa Kisarawe kukamilika kwa asilimia 99. Hatua hiyo imefikiwa, baada ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (DAWASA) kukamilisha ujenzi wa tanki la maji lenye ujazo wa Lita Milioni 6 kukamilika. Mradi huo wenye thamani ya Bilioni 10.6 uliojengwa kwa fedha za ndani za Dawasa unaotoa maji kutoka Tanki la maji la Kibamba hadi Kisarawe. Kuanza kwa mradi huo kutawanufaisha wananchi wengi zaidi na maunganisho mapya 1000 watakao unganishwa maji kwa mkopo na kulipa ndani ya mwaka mmoja. Naibu Waziri wa Maji Jumaa Aweso ameupongeza uongozi wa Dawasa kwa jitihada kubwa walizozifanya ndani ya muda mfupi kwa kuhakikisha maji yanafika katika mji mdogo wa Kisarawe. “Naupongeza uongozi wa Dawasa, Mwenyekiti, Mkurugenzi na watendaji wengine kwa kazi kubwa waliyoifanya ya kuhakikisha wanajenga mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya Bilioni 10.6 kwa fedha za n...

AfDB kuipatia Tanzania zaidi ya Tsh. Tilioni 1

Image
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imepongeza uamuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wa kuhamia Dodoma na kuahidi kuidhinisha kiasi cha dola za kimarekani milioni 455 sawa na zaidi ya shilingi za Kitanzania trilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa Msalato sambamba na ujenzi wa barabara za mzunguko Jijini  humo. Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina ameyasema hayo katika Ofisi za Makao Makuu ya Benki hiyo yaliyopo Abijdan Nchini Ivory Coast wakati wa Mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na kuongeza kuwa benki hiyo itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Rais Dkt John Pombe Magufuli katika kipindi chake cha Uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) lakini pia kwa Tanzania. Amesema Benki hiyo tayari imeshaidhinisha kiasi cha dola za marekani milioni 180 kwa ajili ya ujenzi wa barabara za mzunguko jijini  D...

Serikali yapongeza Juwanata kwa kuanzisha Jumuiya ya wasindikaji Nafaka

Image
Serikali imeupongeza uongozi wa muda wa Jumuiya ya Wasindikaji Nafaka Tanzania (JUWANATA) kwa kukamilisha rasimu ya katiba ya umoja wao. Pongezi hizo za serikali zimetolewa na Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Masoko toka Wizara ya Kilimo Benito Kavenuka wakati wa mkutano maalum wa Juwanata uliofanyika Jijini Dar es Salaam . Kavenuke amesema kuundwa kwa jumuiya ya wasindikaji mazao ya nafaka ni utekelezaji wa azimio la mkutano wa wafanyabiashara ya mazao ya nafaka uliofanyika mwezi Agosti mwaka huu chini ya  Waziri wa Kilimo. “Serikali inaunga mkono Juwanata kwa kutekeleza kwa haraka azimio la mkutano wa Waziri wa Kilimo na wafanyabiashara wa nafaka la kuanzisha jumuiya hii muhimu  kwa ustawi wa viwanda vya mazao ya nafaka.” alisema Kavenuka. Aliongeza kusema serikali itapenda kuona Viongozi wa jumuiya hii wanasimamia viwango vya ubora wa bidhaa za nafaka  zinazalishwa ili kuwa na uhakika wa soko na bei nzuri. Kavenuka amewataka pia kuongeza wigo wa kuwafik...

Saratani ya Matiti yaweza kushika namba moja

Image
Endapo hatua zisipochukuliwa za saratani ya matiti inaweza kushika namba moja kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa nchini. Hayo yanesemwa na Mkurugenzi wa huduma za Kinga ya Saratani katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI) Dkt. Crispian Kahesa alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu mwezi wa uhamasishaji, uelimishaji na uchunguzi wa saratani ambao huadhimishwa kila mwezi oktoba kila mwaka. “Idadi ya saratani ya matiti inaonekana kuongezeka nchini ambapo hivi sasa wanawake wenye umri kuanzia miaka 20 na kuendelea nao wanagundulika kuugua ugonjwa huu”. Alisema Dkt. Kahesa. Alisema kuwa endapo hatua zisipochukuliwa saratani hiyo itazidi kuwa tishio zaidi na kwamba idadi kubwa ya wagonjwa wanaofika hospitalini hapo wanatoka katika maeneo ya mjini ambapo mkoa wa Dar es salaam unaonekana kuongoza. “Tathimini ya miaka 10 iliyopita saratani hii ilikua inashika nafasi ya tano ,hivi sasa ni ya pili kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa,zamani tulikua tunawaona wagonjwa kuanzia...

MAGAZETI YA LEO 31/10/2019

Image